0

TAARIFA YA HABARI KUTOKA RADIO SENGEREMA FM

KUMALIZA   ZIARA.
Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Joseph Kabila amemaliza ziara yake ya kiserikali ya siku tatu hapa nchini na kurejea nchini kwake. 

Akiwa  katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa  Mwl ,Julius  Kambarage Nyerere Jijini Dar es Salaam Rais Kabila ameagwa na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli.

Katika hatua nyingine, mara baada ya kuondoka kwa Rais Kabila, Rais Magufuli   amefanya ukaguzi wa kushitukiza katika sehemu ya kukagulia mizigo na abiria ya uwanja huo upande wa Terminal One ambapo Mwezi Mei mwaka huu alitembelea kwa kushitukiza na kubaini kuwa mashine za ukaguzi (Scanners) zilikuwa hazifanyi kazi.

Mara hii Rais Magufuli amebaini kuwa mashine hizo zinafanya kazi, baada ya kujionea yeye mwenyewe uhalisia wa namna mizigo inavyokaguliwa. 

Hata hivyo amemuagiza Mkurugenzi wa uwanja wa ndege wa Julius Nyerere Bw. Paul Rwegasha kuwachukulia hatua za kinidhamu maafisa wawili walitoa taarifa za uongo pindi alipofanya ukaguzi wa kushitukiza mara ya kwanza.

Na, Mhariri  Twimanye   Chanzo                   Millad ayo


MAJI           
Wananchi wa katika kitongoji cha KABAGANGA kisiwani KOME katika halmashauri ya  Buchosa mkoani MWANZA wameiomba serikali kuwachimbia visima ili kukabiriana  na tatizo lililopo la maji.
Wakielezea hali hiyo wananchi hao wamesema kuwa huwalazimu  kuamka majira ya saa nane za usiku na kurudi nyumbani saa nne za asubuhi hari inayopelekea kukwamisha shughuli za kila siku za maendeleo.
Hata hivyo kwaupande wake mwenyekiti wa kitongoji hicho cha KABAGANGA KATI Bwana  SAMWEL JOHN  amekiri kuwepo kwa hali hiyo.
Na,  Marlesa/ Mhariri   Twimanye Chanzo   Mahojiano.



CHAMA CHA WALIMU
Chama cha Walimu Mkoa wa    Mwanza kimeituhumu ofisi ya mkurugenzi wa Jiji la Mwanza kuhusika na kugushi takwimu za  idadi ya wanafunzi    na kusababisha kuwepo wanafunzi hewa  5559 .
Akisoma tamko la walimu hao katibu wa chama cha  Walimu  Wilaya ya  Nyamagana    Asha Juma  amemtaka mkurugenzi  wa jiji kuwaomba radhi walimu wakuu 62, waliosimamaishwa kazi kwa tuhuma zakuandaa orodha za wanafunzi hewa katika shule zao vinginevyo kitamfikisha mahakamani.
Baadhi ya walimu waliofukuzwa kazi  wamezishangaa takwimu zilizotumika kuwasimamisha   kazi.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa jiji la Mwanza Kihomoni Kibamba  amesema hayuko tayari kuwaomba radhi walimu hao na kwamba  endapo  hawajaridhika na hatua  aliyoichukua      wapeleke mamalamiko ya katika   tume ya utumishi wa walimu.
Chama cha Walimu Wilaya ya Nyamagana kimetishia kwenda mahakamani endapo mkurugenzi wa jiji hilo hatawaomba radhi walimu hao waliosimamishwa kazi na kutengua barua aliyowaandikia.
Na,  Mhariri  Twimanye   Chanzo          TBC.

                   BARABARA.
Wakazi wa Kijiji cha Balatogwa  kilichopo kata ya Mwabaluhi Wilayani Sengerema ,wamelalamikia kitendo cha baadhi ya viongozi waliotoa  ahadi  ya   kukarabati    barabara    itokayo  Mjini  Sengerema   hadi  Ngoma  kwa kushindwa kutekeleza  ahadi hiyo kwa wakati.
Katika mahojiano na Radio Sengerema wananchi hao wamesema licha ya viongozi hao kutoa ahadi ya kutengeneza  barabara  hiyo  kabla ya msimu wa masika kuanza wataikarabati lakini mpaka sasa bado ni kitendawili.
Wamesema kuwa   kwa sasa wamekuwa na mashaka na viongozi hao juu ya kukamilisha ahadi hizo  kwani kiongozi  bora   hujali matakwa ya wananchi wake kwa   hutimiza ahadi mapaema.
Kufuatia malalamiko hayo ya wananchi Radio Sengerema imemtafuta mewenyekiti wa kijiji cha Balatogwa Bwn,Joseph Nzungu John ili kujibu malalamiko hayo ya wananchi ambapo amesema serikali ya kijiji hicho inatarajia kuitisha kikao ili kuitafutia ufumbuzi kero hiyo.
Ubovu wa barabara itokayo Mjini Sengerema hadi Ngoma imekuwa ikilalamikiwa na wananchi kwa muda mrefu sasa bila kupatiwa ufumbuzi wowote.
Na,  Mhariri  Twimanye  Chanzo    Mahojiano.

 KUSIMAMISHWA

Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Mashaka Gambo, amewasimamisha kazi watumishi watatu wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro kwa tuhuma za ubadhirifu wa fedha za uchaguzi wa mwaka 2015.
Watumishi waliosimamishwa kazi  ni pamoja na Bi. Hadija Mkumbwa ambae alikuwa msimamizi wa uchaguzi wa mwaka jana  na kumfuta cheo hicho, Bwana Evansi Mwalukasa aliyekuwa mwekahazina wa halmashauri na bwana Sembeli Sinayo aliyekuwa mwanasheria wa halmashauri.
Maamuzi hayo yamefikia baada yakubainika kuna upotevu wa fedha za uchaguzi takribani Milioni 188 ambazo matumizi yake hayakuwekwa wazi na pia Milioni 20 zilitumika kwa manunuzi ambayo hayakufuata taratibu za manunuzi ya serikali.
Aidha Muheshimiwa Gambo alisema maamuzi hayo yametokana na taarifa aliyokabidhiwa na kamati aliyoiunda yakuchunguza mapato na matumizi ya fedha za halmashauri hiyo na kubaini upotevu huo wa fedha nyingi ambazo zingeweza kusaidia shughuli mbalimbali za uchaguzi katika Wilaya hiyo.
Na,  Mhariri      Twamanye          Chanzo      Dewji.


KIMATAIFA.
Polisi nchini Ujerumani wanawachunguza mume na mke ambao wanadaiwa kumfungia mtoto wao  wa kiume ndani ya nyumba kwa miaka 30, katika jimbo la Bavaria

Mwanamme    huyo wa miaka 43 hajawahi kuonekana hadharani tangu kuacha shule akiwa na miaka 13.

Aidha   Polisi wamesema japo mwanamme huyo yuko shwari kiafya, hata hivyo ameonekana kuwa na mfadhaiko.

Na,  Mhariri  Twimanye  Chanzo    BBC.




KIMATAIFA.
Rais wa Rwanda Paul Kagame amefanya mageuzi madogo ndani ya baraza lake la mawaziri kwa kuunda wizara ndogo inayohusu maswala ya katiba na sheria nyingine.
Mageuzi makubwa yanahusu wizara ndogo mpya iliyoundwa katika wizara ya sheria ikihusu maswala ya katiba na sheria nyingine.
Wizara hiyo ndogo imepewa Bwana Evode Uwizeyimana ambaye wengi nchini   Rwanda walimfahamu kama mkereketwa wa upinzani dhidi ya utawala wa RPF kabla ya kurejea nchini miaka 2 iliyopita akitoka uhamishoni nchini Canada.
Mara baada ya kurejea nchini Bwana Uwizeyimana alijumuishwa katika tume ya Rwanda iliyofanya mabadiliko ya katiba ambapo rais Kagame aliongezewa muda wa kukaa madarakani.
 Rais Kagame amembadilishia wizara Dr Diane Gashumba aliyekuwa waziri wa familia na usawa wa jinsia na kumweka katika wizara ya Afya,wadhifa uliokuwa wazi tangu kufutwa kazi kwa Dr Agnès Binagwaho miezi mitatu iliyopita.
Aidha wizara ya maswala ya nchi za Afrika Mashariki imeunganishwa na wizara ya biashara inayoendelea kuongozwa na François Kanimba.

Aliyekuwa waziri wa maswala ya jumuiya ya Afrika Mashariki Bi Valentine Rugwabiza ameteuliwa kuwa balozi wa Rwanda katika Umoja wa mataifa.

  TAMATI YA TAARIFA YA  HABARI 


Post a Comment

 
Top