0
TAARIFA YA HABARI KUTOKA RADIO SENGEREMA FM

KIFO.

Mwalimu wa shule ya Msingi   Kizugwangoma  Kata ya Mission   Wilayani Sengerema Mkoa mwanza  George Mtaki  amekutwa amefariki  na mwili wake ukiwa babarabani majira ya saa 12.20 asubuhi. 


Mwenyekiti wa Mtaa wa Igogo Kata ya Nyampulukano   Goodluck Daudi amesema alipigiwa simu majira ya saa 12:20 asubuhi kuwa katika eneo lake karibu  na kanisa la Babtisti barabara iendayo Hosipitali teule  ya Wilaya kuna mtu amefariki dunia.

 Bw, Daud amesema kuwa hapo awali mwalimu huyo alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa pumu mazingira waliyomkuta akiwa amepoteza maisha inaonekana wazi kuwa alikuwa akielekea hospitali  kupata matibabu kwa kuwa walimkuta ameshikilia fedha na dawa aliyokuwa akitumia. 

Mgaga mkuu wa Hosipitali teule  ya Sengerema  Sister Mary Jose amethibitisha kupokea mwili huo na baada ya kuuchunguza walikuta hana jeraha lolote katika mwili wake na walikuta maji ndani ya tumbo na inawezekana kwa kuwa alikuwa na ugonjwa wa pumu inaonekana wazi kuwa ndiyo umepelekea kifo chake.
Jeshi la Polisi Wilayani Sengerema  limethitisha kutokea kwa kifo hicho.

BARABARA
Abiria wanaotumia barabara itokayo sengerema kuelekea Ngoma wameilalamikia barabara hiyo kutokana na ubovu hali inayosababisha usumbufu mkubwa wakati wa kusafiri.
Barabara hiyo wameeleza ni kiungo kikubwa katika usafirishaji wa bidhaa mbalimbali hivyo ubovu huo unakwamisha shughuli za maendeleo kwa wakazi wa maeneo hayo.

Kwa upande wake Diwani wa kata ya Igalula Mhe,Onesmo  Mussa  Mashili amesema barabara hiyo  ilisuasua kutokana na ukosefu wa fedha ambapo kwa sasa tayari pesa imekwishapatikana na mkandarasi novemba mwaka huu ataanza ukarabati mara moja ili kuwaondolea adha wakazi wa kata hiyo.
Hata hivyo diwani huyo amemshukuru mkuu wa wilaya ya sengerema bw Emmanuel Kipole   baada ya kuingilia kati  kutokana na mkandarasi  kushindwa kuanza kazi kwa wakati ambapo alipaswa kuanza kazi tangu Octoba 6,mwaka huu  hivyo amemuaru kuanza kazi hiyo mara moja.
Na Veronicah/Paulina         Chanzo;Mahojiano.


WAZEE

Mkuu wa Wilaya  ya  Sengerema Emmanuel Kipole  amezita mamlaka husika ziache  tabia ya kuwatoza  fedha za matibabu wazee  wanapofika hospitalini kupata matibabu.

Kauli hiyo ameitoa Katika Kata ya Kafunzo Halimashauri ya Buchosa Wilayani humo baada ya  Kikundi cha wazee cha kata hiyo kiitwacho UWAKA  kumlalamikiamkuu huyo wa wilaya kutozwa fedha wanapofika kupata huduma za afya kinyume na sera ya wazee.

Amesema kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Taifa imepitisha sheria ya wazee kuanzia miaka 60 kupata huduma bure za matibabu katika Zahanati na hosipitali zote nchini kwa kuzingatia kuwa kundi hilo halina uwezo wa kujihudumia katika swala la fedha za matibabu.

Kipole amesema kuwa zama za kuwatoza wazee zimekwisha hivyo huduma hiyo inapaswa kutolewa bure na mtumishi yoyote wa afya atakaye watoza fedha za  matibabu wazee waliofika kupata matibabu au kuwanyanyasa wazee  wakati wakipata matibau hata vumiliwa na atakuwa amejifukuzisha kazi .
Na,Paulina          Chanzo:Mahojiano.

MAZINGIRA.

Halimashauri ya Wilaya Sengerema  imeagizwa kuunda vikundi vya usafi wa mazingira kila kata kwa lengo la kuondokana na adha ya uchafu unaotokana na kuzalishwa na wananchi wa maeneo mabailimabali katika mji wa Sengerema.


Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Wilaya Sengerema Emmanuel Kipole  alipokutanana na wenyeviti wa mitaa na Madiwani  wanaounda mamlaka ya mji mdogo wa Sengerema  katika kikao cha pamoja kwa lengo la kujadili mambo mbalimbali ikiwemo swala la usafi wa mazinga na ulinzi na usalama.

Amesema suala la usafi wa mazingira ni jukumu la kila raia  hivyo wanapaswa kuwajibika katika swala hilo ili mji  na mazingira yawe safi kwani kwa kufanya  hivyo watatumisha  afya na kuepukana na kukumbwa na magonjwa ya mlipuko hasa kipindupindu.


Na, Said/Paulina                              Chanzo:Kikao


KIMATAIFA                             
Mdahalo wa pili wa wagombea urais wa Marekani Hillary Clinton na Danald Trump umefanyika leo hii.

Kampeni kwa upande wa chama cha Republican ipo katika mtikisiko baada ya kuvuja kwa mkanda wa video wa mwaka 2005 uliyomrekodi Trump akizungumza maneno machafu dhidi ya wanawake.

Ikiwa uchaguzi wa Marekani unatarajiwa kufanyika si zaidi ya mwezi mmoja, idadi kadhaa ya wabunge waandamizi wa chama cha Republican wamejiondoa katika kumuunga mkono bilionea huyo.

Trump mwenyewe amesalia kuwa mkaidi pamoja na miito ya kumtaka ajiondoe katika kinyang'anyiro hicho.
Kabla kuanza mdahalo huo katika ukumbi wa Chuo Kikuu Washington, St. Lous viongozi hao wawili walishindwa kupeana mikono.
Na, Paulina                     Chanzo:DW.

KIMATAIFA         
Serikali ya Ethiopia imetangaza miezi sita ya hali ya hatari nchini kote kufuatia kufanyika maandamano ya wanaoipinga serikali ambayo yamesababisha watu kadhaa kupoteza maisha.

Akizungumza kupitia televisheni, Waziri Mkuu Hailemariam Desalegn amesema machafuko hayo yameathiri mali na kutishia utulivu wa taifa na usalama.

Miji mikubwa na midogo katika eneo la Oromia nchini Ethiopia kumeshuhudiwa vurugu za maandamano ya watu wanaodai uhuru zaidi.

Zaidi ya watu 50, walikufa katika mkanyagamno ulitokea juma lililopita, baada ya polisi kuwafyatulia mabomu ya machozi na risasi kuwawatawanya waandamanaji hao wanaoipinga serikali.
Maandamano yalianza mwaka uliopita kutokana na hofu kwamba mpango wa serikali kuongeza mpaka wa Addis Ababa ungewapokonya baadhi ya wakulima maeneo yao.


MWISHO WA TAARIFA YA HABARI

Post a Comment

 
Top