0
TAARIFA YA HABARI KUTOKA RADIO SENGEREMA FM

TUKUIO.
Jeshi   la polisi   mkoani Pwani  ,limewakamata watoto 22 wa madrasa ya Arahma pamoja na mwalimu wa madrasa hiyo ambae alikuwa akiendesha mafunzo ya kigaidi kwa watoto hao,  Kimarang’ombe ,kata ya Nianjema Bagamoyo.

          
Kwa undani wa habari hii , usikose kufuatilia taarifa hii  katika uchambuzi wetu wa habari kwa kina muda mfupi ujao.

HAKI    ELIMU.
Shirika la  haki   Elimu  na  Kituo  cha  Sheria  na  haki      za Binadamu, wamelaani kitendo cha adhabu ya kikatili aliyopewa mwanafunzi wa shule ya sekondari  ya kutwa ya Mbeya   Sebastian Chinguku na walimu wa shule hiyo.
Akiongea na waandishi wa habari, leo  Mkurugenzi Mtendaji wa Haki Elimu, John Kalage, amesema vitendo kama hivyo vinachangia kwa kiasi kikubwa watoto wengi hususani wa kike kuacha shule, hivyo kukosa haki yao ya msingi ya kupata elimu.
Pia ameishauri serikali juu ya uboreshaji wa utoaji wa taarifa dhidi ya matukio ya kikatili kama hayo yanapotokea.
Mkurugenzi huyo ameongeza kuwa,serikali inatakiwa kuboresha miongozo yake ya kusimamia na kuimarisha nidhamu shuleni na kuhakikisha inazingatiwa na watu wote.
Kwa upande wake Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu, kimepongeza mshikamano uliooneshwa na wananchi katika kukemea ukatili huo.

Na,    Mhariri   Twimanye   chanzo        Mpekuzi

UKOSEFU WA MADARASA
Wanafunzi wa darasa la kwanza hadi la tatu  wa Shule ya msingi Chikomelo iliyopo kijiji cha Ngoma wilaya ya Sengerema wamelazimika  kusomea darasa moja kutokana  shule hiyo kukabiliwa na changamoto ya ukosefu wa madarasa.  
Mwanahabari wetu SAID MAHELA ametembelea katika shule hiyo  na kutuandalia taarifa ifuatayo.
Hayo yamebainika wakati Diwan wa kata ya Ngoma Mh.Onesmo Mussa Mashili alipokuwa akiongea na wananchi kwenye mkutano wa hadhara katika kitongoji hicho.
Mh. Onesmo  amekiri kuwepo kwa tatizo hilo na kuwaomba wananchi kushirikiana kwa pamoja   kujenga vyumba vya madarasa.
Aidha diwani huyo   amewaomba wananchi wa kitongoji  hicho  wahakikishe wanaweka utaratibu mzuri wa kuchangia michango kwa ajiri ya maendeleo ya kitongoji  chao.  
Na,Said /Mhariri  Twimanye         Chanzo  Mkutano.       

WAZEE
Kufuatia tamko la serikali kuwa wazee wote hapa nchini wanatakiwa  kupatiwa matibabu bure, baadhi ya wazee Wilayani Sengerema ,wamepongeza huduma zinazotolewa katika  hospital teule ya wilaya ya Sengerema Mkoani Mwanza.
Wakizungumza na Radio Sengerema, wazee hao wamesema kwa sasa wamekwisha pewa vitambulisho vya kuwatambulisha ili  wakati   wowote watakapohitaji matibabu waweze kupata kwa urahisi  tofauti na hapo  awali hawakuwa na vitambulisho hivyo.
Wameeleza kuwa  hapo awali walikuwa hawapati matibabu bure ,kutokana na  kukosa vitambulisho,  jambo ambalo  limekuwa likisababisha usumbufu mkubwa pindi wanapougua ikiwemo kutopatiwa huduma ya matibabu  kwani hawana uwezo wa kumudu gharama za matibabu. 
Hata hivyo  wameipongeza serikali kwa kutambua uwepo wa  wazee  hapa nchini  na  kuwaomba watumishi wa sekta ya afya waendelee  kuwapa kipaumbele  kwa   kuwahudumia bure  bila kujali itikadi za vyama vya siasa,dini wala kabila.
Na ,Mhoja /Mhariri     Chanzo                   Mahojiano. 
KILELE CHA   MWENGE
Rais Dkt,John Pombe   Magufuli anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika sherehe za kilele cha mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa zitakayozofanyika Bariadi mkoani Simiyu, huku zikitanguliwa na maonyesho ya wiki ya vijana.
Mbali na Rais Magufuli katika kilele hicho, Mke wa Baba wa Taifa Mwl Julius Kambarage Nyerere, Mama Maria Nyerere anatarajia kuhudhuria misa ya maadhimisho ya kumbukumbu ya miaka 17 ya kifo cha mwasisi huyo wa Taifa zitakayofanyika katika   Kanisa la Mtakatifu Yohana mjini Bariadi.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Antony Mtaka amesema maadhimisho ya wiki ya vijana yatafunguliwa rasmi Oktoba 8 hadi 14, mwaka huu na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na wenye Ulemavu, Jenisita Mhagama katika uwanja wa Sabasaba mjini humo
Pamoja na hayo     Mtaka amesema maadhimisho hayo yataenda sambamba na kongamano la vijana.ambapo  katika kongamono hilo kutajadiliwa mada mbalimbali zinazoihusu jamii, ikiwemo kupinga mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi.
Na Veronica/Mhariri   Twimanye          Chanzo Mtembezi.

 KIMATAIFA 
Idadi ya watu waliopoteza maisha kutokana na kimbunga Matthew imezidi  kuongezeka na  kufikia    watu 478, wakati taarifa zikiingia kutoka maeneo ya ndani ambayo hapo awali yalikuwa yamekatika kutokana na dhoruba kali. 
Wakati idadi hiyo ikiongezeka, mashirika ya serikali na kamati tofauti zimekuwa zikitofautiana juu ya idadi kamili ya watu.
Ripoti iliyoripotiwa na shirika la habari la Reuters na kutolewa na maafisa wa asasi za kiraia katika ngazi ya mitaa imethibitisha idadi ya vifo 478  huku  Shirika la ulinzi wa raia la Haiti limesema watu 271 wamefariki kutokana na dhoruba  na wengine 61,500 wakibakia katika mkazi.
Kimbunga Matthew pia kimeipiga Florida katika upepo wa kilometa 205 kwa saa na kuhatarisha uharibifu zaidi wa miundombinu.

Na,  Mhariri Twimanye   Chanzo     Dw.


KIMATAIFA
Rais wa Colombia Juan Manuel Santos ameshinda tuzo ya amani ya Nobel kwa mwaka  huu, licha ya wapiga kura kukataa mkataba wa kihistoria wa amani baina ya serikali yake na waasi wa FARC uliofikiwa mwezi uliopita wa kumaliza miaka 52 ya vita.
Santos ameahidi kufufua mpango wa amani licha ya kukataliwa na raia.
Mwenyekiti wa kamati ya tuzo hiyo Kaci Kullmann wakati  akimtangaza mshindi Santos wa tuzo hiyo,  tuzo hii  pia ni heshima kwa watu wote wa Colombia ambao licha yamatatizo makubwa na ukiukwaji, hawajapoteza matumaini ya kupata amani.   
Tuzo hiyo yenye thamani ya dola za kimarekani laki tisa na elfu 30 itawasilishwa mjini Oslo Disemba 20 mwaka huu.













Post a Comment

 
Top