0
  MAFANIKIO YA RAIS MAGUFULI.               
Baadhi ya wakazi wa Wilaya ya Sengerema  wamesema  Rais Dkt,John Pombe Magufuli amefanya mageuzi makubwa  ya  kimaendeleo  hasa  katika nyanja  ya elimu  na afya  tangu  alipoingia madarakani Novemba 5 mwaka jana.
Hayo wameyasema katika mahojiano  maalumu  na Radio Sengerema  yaliyoangazia  mambo   aliyofanya   Rais Dkt,Magufuli  tangu  alipoapishwa na kuanza rasmi majukumu yake ya kuiongoza Tanzania Novemba  5 mwaka jana zikiwa zimesalia siku chache   kutimiza mwaka mmoja wa uongozi wake.

Wameeleza kuwa pamoja na mambo mengine Rais Magufuli amesaidia kuokoa kiasi kikubwa cha fedha walizokuwa wakilipwa watumishi hewa  ambao hawafanyi kazi yoyote ya  kuliingizia  kipato    taifa  na kuzielekeza  katika  shughuli  za kimaendeleo.

                                   KILIMO
Wakulima wameshauri kukagua mbegu wakati  wa kununua katika maduka ya pembejeo za kilimo ili kubaini ubora wa mbengu na kuhakiki  muda wa matumizi kama umekwisha.
Akifanya mahojiano na redio sengerema ofisini kwake afisa mazao  wilaya ya sengerema bwana BERNAD MYATIRO ameeleza kuwa wakulima wengi hushindwa kukagua mbegu kama ina ubora ikiwemo muda wa kumalizika kwa nguvu ya mbegu hiyo na uwepo wa nembo ya tosic ambayo huonyesha kama mbegu hiyo imeruhusiwa kisheria na  kununu mbegu ambayo haioti na kumsababishia hasara mkulima.
         
Aidha bwana MYATIRO ameongeza kuwa ni vyema maafisa ugani wa kata na vijiji kutumia muda wao mwingi kuwaelimisha wakulima namna ya kutambua mbegu bora hususani katika kipindi hiki cha kilimo ambacho wakulima wengi huhitaji mbegu kwa ajili ya kilimo ili kuepuka hasara kubwa ambayo wakulima wanaweza kuepuka .
Hata hivyo Bwana MYATIRO amewataka wakulima kulima mazao ya muda mfupi na yanayoweza kukabili ukame kulingana na hali ya hewa ilivyo hivi na mvua kuchelewa kuanza kunyesha kama vile mtama na mihogo na mahindi aina ya DK,situka,sidiko amabazo zinaweza kukomaa ndani ya siku 75 mpaka skiu 110.

                                             TCU
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ameitaka Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU), kuhakikisha programu za masomo zinazoanzishwa na vyuo vikuu nchini zinazingatia mahitaji ya Taifa na soko la ajira.
Majiwali ametoa  agizo hilo leo wakati wa kilele cha maadhimisho ya miaka 55 ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).

Amesema hivi sasa kuna baadhi ya vyuo nchini ambavyo vinatoa programu ambazo haziendani na mahitaji halisi ya Taifa pamoja na soko la ajira.

Kwa upande wake MKUU wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Rais mstaafu Jakaya Kikwete amekitaka chuo kikuu hicho kilinde hadhi yake ya kuendelea kuwa kiongozi katika utoaji wa elimu bora, ambayo itasaidia taifa kuwa na wataalamu wenye kusaidia kutatua changamoto mbalimbali zinazoikabili kijamii.

                               MKATABA
Kampuni ya Sonalika international Tractor limited ya India imesaini mkataba wa makubaliano na kampuni ya Quality Group kwa ajili ya kuunda trekta za kilimo hapa nchini.

Mkataba huo unakadiliwa kuwa na thamani ya takriban Sh bilioni 50 mpaka 100 na umelenga kuongeza upatatikanaji wa bidhaa hiyo kwa urahisi sanjali na punguzo la bei ili kuwanufaisha wakulima wadogo, wakati na wakubwa.

Ofisa Masoko wa Qualiy Group Timoth Shuma amesema Undaji wa trekta hizo unatarajiwa kuanza mapema mwaka ujao huku zikiwa na punguzo la bei la zaidi ya asilimia 30.
                             KIMATAIFA                         
Shambulio la usiku katika mji wa Mandera nchini Kenya limetekelezwa na wanamgambo wasio al-Shabab, kwa mujibu wa mratibu wa usalama wa eneo la kaskazini mashariki mwa Kenya Bw Mohamud Saleh.
Kundi la Al-Shabab Somalia tayari limekiri kuhusikana shambulio hilo dhidi ya nyumba ya malazi , kama tulivyoarifu awali.
Lakini Bwana Saleh amesema kutokana  na kuwa mpaka na Somalia hufungwa kuanzia usiku hadi alfajiri , hakuna namna kwa washambuliaji kuvuka mpaka huo.
Ameongeza kuwa uchunguzi wa awali umedhihirisha kuwa shambulio hilo la saa tisa alfajiri lilitekelezwa na magengi ya wahalifu walio na itikadi kali waliopo katika mji wa Mandera ambao wametumia vilipuzi vinne kuilipia nyumba hiyo ya malazi.
Watu 12 wameuawa baada ya watu wenye silaha kushambulia nyumba hiyo ya malazi mjini Mandera.
Msemaji wa serikali ya Kenya Eric Kiraithe amesema watu sita wameokolewa kutoka kwenye hoteli hiyo ya Bishaaro.


                               KIMATAIFA             
Mratibu wa shughuli za msaada za Umoja wa Mataifa, Stephen O'Brian, amezikosoa pande zote zinazohusika katika mzozo wa vita mjini Aleppo, siku mbili baada ya kumalizika muda wa kusitisha mapigano.
Afisa huyo amesema serikali ya Syria na waasi wanaoipinga, walizuia watu kuondoka sehemu zilizozingirwa na upelekaji wa mahitaji muhimu kwa watu wanaouhitaji.
O'Brian amesema kutokana na hali hiyo wameamua kuacha mpango wa kuwapelekea msaada watu waliojeruhiwa katika mji huo wa kaskazini mwa Syria.
Aidha, mratibu huyo wa shughuli za msaada amesema ni jambo la kukasirisha kuona pande zinazopigana, zikiweka mbele maslahi ya kisiasa na ya kijeshi, na kuwapuuza wagonjwa, watoto na vikongwe wanaoteseka.
Umoja wa Mataifa umeshindwa kufikisha misaada katika sehemu ya Mashariki ya Aleppo iliyo chini ya udhibiti wa waAsi tangu mwezi Julai.
                  MICHEZO NA BURUDANI
Kocha George Lwandamina amemalizana na Yanga kwa maana ya mazungumzo lakini amerejea nchini mwao bila ya kusaini mkataba na Yanga.

Kocha huyo ameondoka nchini leo alfajiri kurejea Lusaka Zambia kwa ajili ya kukamilisha masuala ya kifamilia.

Lwandamina ndiye anatarajiwa kuchukua nafasi ya Kocha Hans van der Pluijm raia wa Uholanzi.

Kocha huyo wa zamani wa Zesco, alitua nchini juzi na kufanya mazungumzo na uongozi wa Yanga.
                   =======      =======   =======
Mshambuliaji nyota wa FC Barcelona, Luis Suarez ameteuliwa kuwa mwanasoka bora wa dunia kwenye La Liga.

Tuzo hiyo ni kwa ajili ya msimu wa 2015-16 kwa wachezaji wa La Liga.

Tuzo hiyo hujumuisha mchezaji anayezungumzwa au aliye gumzo zaidi katika sehemu mbalimbali duniani lakini anatokea kwenye ligi ya  La Liga.

                       =====   ======    ======

                                     BIASHARA                          
Kuelekea uchumi wa viwanda nchini, serikali imefanikiwa kufufua na kuanzisha viwanda ambapo kwa sasa vinavyofanya kazi vipo zaidi ya 52,000. Sekta hiyo pia imetajwa kuwa inatarajia kukuza uchumi wa watanzania asilimia 40.

Hayo yamesemwa leo na Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maonesho ya viwanda Tanzania yanayotarajiwa kufanyika katika viwanja vya sabasaba jijini Dar es Salaam kuanzia Disemba 7 hadi 1, 2016.

Aidha, Mwijage amesema Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kupitia taasisi yake ya Mamlaka na Maendeleo ya Biashara Tanzania, imeandaa maonesho yatakayokutanisha wadau wa sekta ya viwanda kwa lengo la kutangaza pamoja na kujadili fursa za masoko ya ndani na nje ya nchi.

Amesema maonesho hayo pia yatatoa taswira ya juhudi za ujenzi wa viwanda katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita.




Post a Comment

 
Top