0
TAARIFA YA HABARI KUTOKA RADIO SENGEREMA

MAKUBALIANO
Serikali za Tanzania na Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo zimeahidi kuendeleza ushirikiano katika nyanja mbalimbali za kiuchumi ikiwemo sekta ya uchumi ya nishati ya mafuta pamoja na biashara.

Akizungumza na waandishi wa habari Ikulu jijini Dar es salaam rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt, John Pombe Magufuli mara baada ya  uwekaji sahihi mikataba ya makubaliano ya utafutaji na uendelezaji wa mafuta katika ukanda wa magharibi mwa Afrika mashariki  katika ziwa Tanganyika.
Rais Magufuli amesema Tanzania ni sehemu salama  ya uwekezaji ambapo ametoa wito kwa wafanyabiashara na serikali ya Congo kuja nchini kuwekeza ili kukuza uchumi wa  nchi zote mbili.
Clip  Rais Magufuli 1……..
Kwa upande wake rais wa Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo  Joseph Kabila amesema nchi yake itaendelea kuitumia bandari ya Dar es salaam na kuendeleza ushirikiano kati nchi yake na Tanzania.
Na Veronica/Mhariri    Twimanye                            Chanzo TBC.

MWILI.
Hali ya  taharuki imetanda katika  eneo la   Busaka   Wilayani Chato Mkoani Geita baada ya kaburi la mtu aliyezikwa miaka 31   iliyopita kufukuliwa na  ndugu  wa marehemu  na kwenda kuzikwa    katika  kijiji  cha Nyitundu  Wilayani Sengerema Mkoani  Mwanza bila taarifa yoyote kwa  baadhi  ya  ndugu wa marehemu huyo.
Msikilizaji  usikose kusikiliza taarifa hii muda mfupi ujao katika uchambuzi wetu wa habari kwa kina.


ONYO.
Kamati ya Maudhui ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imetoa onyo kali kwa kituo cha Televisheni cha Clouds sambamba na kukifungia kwa miezi mitatu kipindi cha Take One kinachorushwa na Kituo hicho.

Makamu mwenyekiti wa kamati hiyo Method Mapunda amesema sababu ya kukifungia kipindi hicho, ni kutokana na ukiukwaji wa kanuni za utangazaji za mwaka 2005, kwa kumhoji na kurusha kipindi cha mtu kinachohamasisha biashara ya ngono,   na kutolinda maadili ya watoto.

Aidha imeelezwa kuwa  sababau ya kufungiwa kipindi hicho ni  mahojiano   kati ya mtangazaji wa kipindi hicho ambayo  yalirushwa Agost 09 mwaka huu  saa 3.00 usiku na kurudiwa kesho yake.  


Na, Mhariri  Twimanye   Chanzo         Mpekuzi.



USALAMA BARABARANI.
Kamanda mkuu  wa  usalama   barabarani wilayani Sengerema mkoani mwanza  Inspector Hamis Wembo amewataka waendesha pikipiki wote kuzingatia uvaaji wa kofia ngumu wakati wa safari zao.
Amesema hayo wakati akizungumza na Radio Sengerema ambapo   amesema  nimarufuku kuendesha pikipiki bila kuvaa kofia ngumu kwa watu wote pasipo kujali kuwa ni waendesha bodaboda ili kujikinga na ajari.  
Sanjari na hayo amesema kuwa   waendesha bodaboda wanatakiwa kuwa na kofia mbili ikiwa moja ya dereva na nyingine  ya abiria .
Pia  amesema kuwa uvaaji wa kofia ngumu ni moja ya sheria zilizo pangwa katika kuzingatia usalama barabarani ili kuepukana na adhabu zilizo pangwa  na serikali  na kwamba kwa yule atakaye vunja sheria  atatozwa  faini.ya shilingi elfu thelathini.
Hata hivyo    amewataka waendesha pikipiki kuzingatia sheria hiyo ya uvaaji kofia ngumu  pamoja na abiria  kupenda kuvaa kofia hizo kamakinga ya ajari.   
Na arafa /Mhariri  Twimanye                           chanzo;mahojiano.
KONGAMANO.

Makamu wa Rais Mh, Mama Samia Suluhu Hassan amewahakikishia Wanasayansi Watafiti waliopo nchini kuwa Serikali ya Tanzania inatambua mchango wao  na wataendelea na juhudi za kuwalinda kwani ni nguzo muhimu ya kufikia malengo ya milenia katika Nyanja mbalimbali ikiwemo Uchumi, Afya, Elimu na Maendeleo endelevu.
Makamu wa Rais   ameyasema hayo mapema leo Jijini Dar es Salaam wakati alipozindua rasmi Kongamano la 30 la Kimataifa la Wanasayansi Watafiti lililoandaliwa na Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) ambalo ni la siku tatu kuanzia  Oktoba 4 hadi 6 mwaka huu.
Akiwahutubia Wanasayansi hao watafiti zaidi ya 300 kutoka Tanzania na Mataifa ya nje,  amesema kuwa Taifa bila watafiti hakuna maendeleoo hivyo uwepo wa watafiti hao ni kielelezo tosha cha kufikia maendeleo. 
Akiwaondoa hofu wanasayansi watafiti hao, Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu amebainisha kuwa, Serikali imesikitishwa na tukio lililotokea hivi karibuni la kuchomwa moto baadhi ya watafiti huko Mkoani Dodoma kuwa ni la kinyama na halivumiliki na sheria itachukua mkondo wake na wahusika wote watafikishwa mikononi mwa sheria.
Kwa upande wake Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mh. Dk. Hamisi Kigwangalla katika mkutano huo amebainisha kuwa,  Wizara yake inashirikiana bega kwa bega na wanasayansi  hao.

Na,   Mhariri   Twimanye       Chanzo            Dewji.
KIMATAIFA.
Marekani imesitisha mazungumzo yake na Urusi juu ya kurejelea kwenye usitishaji mapigano Syria na ushirikiano wa kijeshi dhidi ya makundi ya siasa kali nchini Syria.
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya nje ya Marekani, John Kirby, amesema uamuzi huo unatokana na kushindwa kwa Urusi kuheshimu ahadi zake, na pia kutoonesha nia ya kuulazimisha utawala wa Syria kutekeleza mambo ambayo awali Urusi ilikuwa imeyakubali.
Taarifa ya Marekani juu ya kusitishwa  kwa mazungumzo hayo  na ushirikiano na Urusi iliyotolewa   inagusia pia mashambulizi makali dhidi ya maeneo ya kiraia, miundombinu na hospitali katika mji wa Aleppo.  
Na,    Mhariri  Twimanye  Chanzo        DW.

KIMATAIFA.
Shirika la Kuhudumia Watoto la Umoja wa Mataifa, UNICEF, na Benki ya Dunia wanasema kuwa watoto milioni 385 duniani wanaishi kwenye ufukara wa kutisha.
Taarifa iliyotolewa   na taasisi hizo za kimataifa inasema watoto kwenye maeneo ya Afrika   kusini mwa Jangwa la Sahara na kusini mwa Asia, hasa India, ndio walio kwenye hali mbaya zaidi.
Mwaka 2013, ilikisiwa kuwa asilimia 19.5 ya watoto kwenye mataifa yanayoendelea walikuwa wakiishi kwenye familia ambazo zilikuwa zinapata dola 1 na senti 90  pekee za Kimarekani kwa siku, kwa mujibu wa ripoti hiyo.
Mkurugenzi Mtendaji wa UNICEF, Anthony Lake, anasema watoto wadogo   ndio wenye kuumizwa zaidi na ufukara huo, unaodumaza ukuwaji wao wa kiakili na kimwili.

Na,  Mhariri  Twimanye      Chanzo      DW.
MISHO WA TAARIFA YA HABARI









Post a Comment

 
Top