TAMKO LA
RAIS
Rais Dkt, John Pombe Magufuli amewataka wanasiasa nchini kutotumia siasa katika maafa ya Kagera yaliyotokana na tetemeko la ardhi, na badala yake waungane
kutoa midaada ya hali na
mali kwa waathirika .
Rais
Dkt ,Magufuli ameyasema hayo ikulu jijini Dares salam wakati
waziri wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania mheshimiwa kassim Majaliwa Kassim akimpa taarifa ya maafa yaliyotokana na tetemeko la ardhi Mkoani Kagera
na kuwataka wanasiasa nchini kutotumia maafahayo kisiasa.
Pia Rais ametoa onyo kwa watu wote wasiokuwa na mapenzi mema
wanaotumia maafa hayo ya kagera
kukusanya fedha kutoka kwa watu
mbalimbali , na kuvitaka vyombo vya
dola kuingia kazini na kuwakamata
wahusika wote aliyowaita matapeli.
Katika hatua nyingine
Rais Magufuli ametoa wito
kwawananchi wa kagera
kutobweteka na kusubiri
misaada ya serikali na kuwataka
kujipanga kufanya kazi na kwamba serikali
itafanya yale yaliyondani ya
uwezo wake.
Na, Mhariri
Twimanye Chanzo ITV.
GEITA
Wasamaria wema kwa kushirikiana na jeshi la jadi sungusungu kata ya Kalangalala halamashauri ya mji wa Geita
wamemtia mbaroni kijana anayedaiwa kukutwa katika nyumba ya kulala wageni akifanya
mapenzi na mwanafunzi wa kidato cha nne.
Mwaandishi
wetu YOSEPH MASOTA kutoka Mkoani Geita anaarifu.
kijana huyo philibert
juliasi(26)mkazi wa kijiji cha kayenze alikamatwa saa 4:30 usiku akiwa na mwanafunzi
huyo mwenye umri wa miaka 16 wa kidato cha nne(jina tunalihifadhi) shule ya
sekondari mwatulole.
Baada kukamatwa julias
pamoja na mwanafunzi huyo walifikishwa ofisi ya sungusungu,na ikawa
hivi wakati wakihojiwa na katibu wa sungusungu abeli richard.
kwa upande wake
mtuhumiwa alidai kuwa alianza kufahamiana na binti huyo baada ya kwenda kwake
kurusha muziki kwenye simu,na hadi anakamatwa alikuwa hajui kama ni mwanafunzi.
mama mzazi wa mwanafunzi
huyo,fortunata chambala anasema mtoto wake alitoweka nyumbani katika mazingira
ya kutatanisha tangu jumatatu iliyopita hadi alipopata taarifa za mwanae
kukamatwa gesti.
licha ya serikali kutilia mkazo suala la elimu
sanjali na kuwachukulia hatua wanaokwamisha mkazo huo,baba mzazi wa mtoto
charles pastory akaomba suala hilo lisifikishwe kwenye vyombo vya sheria badala
yake kufanyike mazungumzo,hali ambayo ilipingwa na katibu wa sungusungu ambaye
aliita askari polisi ili kumchukua mtuhumiwa huyo.
mwandishi wa habari hizi
alishuhudia askari polisi wa wilaya ya geita,wakiondoka na mtuhumiwa pamoja na
mwanafunzi huyo kwa ajili ya kwenda kuwachukua maelezo kwa hatua zaidi za
kisheria.
Na, Yoseph
masota /Mhariri Twimanye chanzo
Tukio.
PAMBA.
Wakulima
wa zao la pamba katika kijiji cha NGOMA
wilaya ya Sengerema mkoa wa MWANZA
Wameiomba serikali kurudisha mizani ya
zamani ya Lula kwani iliopo kwa sasa wamedai
kuwa inawapunja.
Mwanahabari wetu
Said
Mahela anahabari kamili.
Kauli
hiyo imetolewa na wakulima wa
pamba kwenye mkutano wa hadhara
ulioitishwa na diwani wa kata hiyo mh,ONESMO MASHILI ambapo
wamesema kuwa, uwepo
wa mizani hiyo imewakatisha tamaa kulima zao hilo.
MH, Mashili
ambaye ni diwani wa kata ya ngoma ameiomba serikali kutatua tatizo la kubadilishwa kwa mizani inayotumika kwa sasa katika kata yake ama itoe
semina juu ya utumiaji wa mizani hiyo kwa wakulima wa pamba ili wawe na
uelewa wa kutumia mizani mipya iliyopo.
Kwa upande wake LAZARO CHUMU Afisa mtendaji wa kata hiyo
amewaomba wakulima wa zao la pamba kununu mbegu iliyo bora na serikali
inatalajia kutoa mbegu kuanzia Novemba 15
mwaka huu.
Hata
hivyo , amewaomba wakulima kuandaa
mashamba yao mapema kwani msimu
wa kilimo umekaribia.
TAASISI.
Waziri
wa afya maendeleo ya jamii ,jinsia wazee na watoto Ummy Mwalimu ameyataka mashirika yasio ya
kiserikali kufanya kazi kwa mujibu wa usajiri wake, badala ya kujiingiza katika
masuala ya siasa.
Waziri
Ummy mwalimu ametoa kauli hiyo katika
mkutano wake na bodi ya uratibu wa
mashirika yasiyokuwa ya kiserikali
ambapo amesema kuwa zipo tarifa
za kuwepo kwa baadhi ya mashirika hayo kujihusisha na masuala ya kisiasa.
Awali
mwenyekiti wa bodi hiyo Nichorus
Zacharia ameiomba serikali kusimamia taasisi binafsi zinazoenda kinyume cha maadili zifutwe.
Na, mhariri
Twimanye chanzo TBC.
KIMATAIFA.
Serikali ya Sudan Kusini imekanusha madai ya ufisadi yaliyotolewa
kwenye ripoti ya shirika moja la Marekani kwamba madai hayo ya ufisadi ,
miongoni mwa maafisa wa ngazi ya juu nchini humo wanayumbisha pia mchakato wa
amani wa nchi hiyo.
Ripoti hiyo
inaeleza jinsi vigogo wanavyojilimbikizia mali huku wananchi wa kawaida
wakiteseka kutokana na madhila ya vita.
Msemaji wa
rais Salva Kiir, anasema madai hayo
hayana msingi wowote na kuwa mataifa ya magharibi yanataka kuchochea mapinduzi
ya serikali yake.
Na, Mhariri
Twimanye chanzo BBC.
KIMATAIFA
Serikali ya Zimbabwe imewaonya waandamanaji wasishiriki kamwe maandamano
kwenye mji mkuu Harare.
Polisi
wametoa onyo wakisema kuwa wale watakaokamatwa kwa kushiriki maandamano hayo
watafungwa hadi mwaka mmoja.
Kumekuwa na maandamano ya kila mara miezi ya
hivi karibuni nichgini Zimbabwe yanayotaka kufanywa mabadiliko katika upigaji
kura na kuondolewa madarakani kwa Rais Robert
Mugabe.
Na,
Mhariri Twimanye Chanzo BBC.
NA HUO NDIO MWISHO WA
TAARIFA YA HABARI KUTOKA RADIO SENGEREMA
FM.
KWA TAARIFA NYINGINE YA HABARI USIKOSE
KUJIUNGA NASI KESHO SAA KUMI KAMILI
JIONI.
Post a Comment