TAARIFA
YA HABARI KUTOKA RADIO SENGEREMA.
ZAHANATI.
Zahanati ya kijiji cha Balatogwa iliyopo kata ya Mwabaluhi Wilayani Sengerema inakabiliwa na ukosefu wa vifaa tiba ikiwemo hadubini, hali
ambayo inawalazimu wakazi wa kijiji
hicho pindi wanapohitaji kupatiwa vipimo kutembea umbali wa kilomita saba
kwenda Hospitali Teule ya Wilaya
ya Sengerema kufuata vipimo hivyo.
Katika mahojiano na
Radio Sengerema baadhi ya wakazi wa kijiji hicho wamesema kuwa hali hiyo
inawapa usumbufu mkubwa na kwamba licha
ya kuwepo zahanati hiyo katika kijiji chao , hawanufaiki na matunda yake kutokana na kukosa vifaa tiba.
Evanjelista
Mbuke ni muuguzi wa
zahanati ya kijiji cha Balatogwa amesema pindi inapotokea watu wengi wanahitaji
vipimo hukosa vipimo kwa sababau ya changamoto ya vifaa hivyo.
Clip
Muuguzi Balatogwa…..
Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Zahanati hiyo Timoth Mashauri amekiri kuwepo kwa ukosefu wa
vifaa tiba katika zahanati hiyo na kuiomba serikali kufanya jitihada za
makusudu kupeleka vifaa hivyo ili kuwaondolea usumbufu wanaoupata wananchi.
Na, Mhariri
Twimanye Chanzo Mahojiano.
UKOSEFU WA SHULE
Kata ya Ibisabageni wilayani Sengerema inakabiliwa na
ukosefu wa shule ya sekondari , hali inayopelekea wanafunzi wa kata hiyo kutembea
umbali mrefu kwenda kusoma kwenye shule za kata jirani.
Kauli hiyo imetolewa na
Diwani wa kata ya Ibisabageni Mh, Jumanne Masunga ambapo
amesema wamekwishaanza jitahada za
ujenzi wa vyumba vya madarasa ili kuwaondolea wanafunzi adha ya kwenda shule za
kata jirani.
Hata hivyo Masunga amewaomba wenyeviti wa vitongoji vyote vilivyopo kwenye
kata yake wachangishe michango kwa wananchi ili zoezi la ujenzi liweze
kukamilika haraka iwezekanavyo ili kuwarahisishia wanafunzi mazingira ya
usomaji.
Na
Veronica /Mahariri Twimanye Chanzo Mahojiano.
KUPANDA MITI
Mkuu wa wilaya ya Busega mkoani Simiyu Tano Mwela
amewaagiza wataalamu wa mashamba na
watendaji wa mashamba wilayani humo kuwa na orodha maalumu ya wakulima wote wa
maeneo yao na kuhakikisha kila familia inalima hekali nne, ikiwa hekali mbili
ni za chakula na mbili za mazao ya biashara.
Ametoa agizo hilo
wakati akizindua kampeni ya upandaji miti
wilayani humo inayojulikana kwa jina la mti wangu ambapo amewahimiza wakazi hao kupanda miti kwa wingi ili
kuepuka majanga yanayoweza kutokea.
Miti aina mbalimbali
imezinduliwa wilayani humo ambapo miti zaidi ya milioni 2 inatarajiwa kupandwa
kwa kila mwaka ili kurudisha uoto wa asili ambao ulikuwa umeanza kupotea
kutokana na ukataji wa miti ovyo.
Aidha wilaya hiyo
imepanga kupanda miti ya matunda 200 pamoja na miti mingine inayowawezesha
kupata mbao na kivuli.
Na
Veronica/Mhariri Twimanye Chanzo TBC.
TUKIO
Video ambayo inadai
kuonyesha tukio la mwanafunzi huyo akipigwa imesambaa mtandaoni Tanzania na Kenya.
Kupitia taarifa, Bw Nchemba, amesema uchunguzi wa awali
unaonesha tukio hilo lilitokea katika shule ya upili ya Mbeya Septemba. 28 mwaka huu ambapo Walimu hao walikuwa wakifanya mafunzo kwa
vitendo.
Anasema mwalimu mmoja
alikuwa amewapa wanafunzi zoezi la Kingereza lakini baadhi ya wanafunzi
wakasusia kulifanya na ndipo mwalimu mmoja alimpiga kofi kijana na kijana akahoji kwanini
anampiga ndipo walimu wakamchukua na
kumpeleka chumba cha walimu na kuanza kumpiga.
Tangu kutokea kisa hicho, inaarifiwa kwamba mwanafunzi huyo hajaonekana shuleni
tena.
KIMATAIFA.
Watu sita wameuawa baada ya watu wenye silaha kushambulia mtaa
mmoja mjini Mandera, kaskazini mashariki mwa Kenya.
Taarifa zinasema washambuliaji hao wamevamia eneo lenye nyumba
za makazi Bulla usiku wa manane.
Gavana wa jimbo la Mandera
Ali Roba ameandika kwenye mitandao
ya kijamii kwamba watu 6 wameuawa na
mmoja kujeruhiwa.
Amesema watu 27 kati ya 33 waliokuwa kwenye ploti hiyo
wameokolewa na maafisa wa usalama.
Kituo kimoja cha redio kinachohusishwa na kundi la al-Shabab
kimesema wanamgambo hao ndio waliotekeleza shambulio hilo.
Gazeti la Standard nalo
linasema walioshambuliwa walirusha guruneti kwanza na kisha wakaingia ndani na
kufyatulia risasi waliokuwemo.
Eneo la Mandera limekuwa
likishambuliwa mara kwa mara na wapiganaji wa al-Shabaab kutoka Somalia.
Kenya ilipeleka vikosi vyake vya jeshi nchini Somalia mwaka wa 2011
ikitaka kuzima mashambulizi ya mara kwa mara na kuisaidia serikali inayoungwa
mkono na Umoja wa Mataifa.
Kundi la al-Shabab mara kwa mara hutekeleza mashambulio nchini
Kenya ikiwemo mauaji ya watu 67 katika maduka ya Westgate mjini Nairobi mwaka
wa 2013.
MWISHO WA TAARIFA YA HABARI
Post a Comment