WIZI WA DAWA
Mfamasia wa Wilaya ya
Sengerema Mkoani Mwanza Bw,KENETH JOHN MAYENGO amekamatwa na jeshi la polisi
kwa tuhuma ya kuiba na kusafilisha dawa
kinyume na sheria.
Akithibitisha tukio hilo
mkuu wa wilaya ya sengerema Bw,EMMANUEL
KIPOLE amesema dawa hizo zilichukuliwa na mfamasia huyo jana majira ya saa
saba katika stoo ya dawa na kumkabidhi dereva bodaboda kwa ajili ya kwenda kuziuza.
Redio sengema
imemtafuta mkurugenzi wa wilaya ya sengerema Bw,MAGESA MAFULU BONIFASI ambae
ni mwajili wake na kueleza kusikitishwa
na kitendo hicho..
ZIARA.
Waziri wa kilimo mifugo na uvuvi ambaye pia ni mbunge
wa jimbo la buchosa Dkt. Charles Tizeba ameahidi kutekeleza
ahadi yake ya kujenga zahanati kila kijiji kama alivyoahidi kipindi cha
uchaguzi kabla ya kukamilika kwa miaka yake mitano kumalizika.
Kauli hiyo ameitoa katika mkutano wa hadhara
uliofanyika katika kijiji cha Luholongoma
kata ya Kafunzo halmashauri ya Buchosa.
Katika kufanikisha ujenzi huo wa zahanati amesema atashirikiana na
wananchi ambapo wao watachangia mchanga na kokoto ambapo yeye atahakikisha
anakamilisha ujenzi huo wa zahanati.
Tizeba amesema amechoka kuona wananchi wakihangaika kutafuta huduma za afya
umbali mrefu hivyo atahakikisha anakamilisha ili kuwaondolea adha wananchi.
MISITU
Kikosi cha Kufuatilia na Kuzuia Uharibifu wa Misitu cha
Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania kimefanikiwa kukamata lori lenye namba za
usajili T 676 ANQ lililokuwa
likisafirisha mbao kinyume cha sheria huku zikiwa zimefichwa kwa kufunikwa na
bidhaa mbalimbali ikiwemo sabuni.
Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam Kaimu Afisa Habari wa Wakala huyo, Nurdin Chamuya amesema baada ya kupata taarifa hizo vikosi hivyo vilifika eneo la tukio na kufanya mahojiano ambapo mmoja kati ya wahudumu wa lori hilo alieleza kuwa lori hilo lilitokea Mkoani Kigoma na kwamba lilikuwa limepakia mzigo wa sabuni na chupa za maji zilizotumika.
Chamuya ametoa wito kwa wananchi wote nchini kushirikiana na Serikali katika uhifadhi na ulinzi wa rasilimali za misitu na kuacha fikra potofu kuwa kazi hiyo ni ya Serikali pekee na taasisi zake kwakuwa faida zake hunufaisha jamii yote.
Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam Kaimu Afisa Habari wa Wakala huyo, Nurdin Chamuya amesema baada ya kupata taarifa hizo vikosi hivyo vilifika eneo la tukio na kufanya mahojiano ambapo mmoja kati ya wahudumu wa lori hilo alieleza kuwa lori hilo lilitokea Mkoani Kigoma na kwamba lilikuwa limepakia mzigo wa sabuni na chupa za maji zilizotumika.
Chamuya ametoa wito kwa wananchi wote nchini kushirikiana na Serikali katika uhifadhi na ulinzi wa rasilimali za misitu na kuacha fikra potofu kuwa kazi hiyo ni ya Serikali pekee na taasisi zake kwakuwa faida zake hunufaisha jamii yote.
MSAADA
MKUU wa Wilaya ya Kakonko Kanali Hosea Ndagala ameipongeza idara
ya Afya Wilayani Kakonko kwa jitihada ya kupungua kwa vifo vya mama na
mtoto kutoka vifo 404 Kati ya vizazi hai 100,000 kwa mwaka kutokana na wadau wa
Afya kuchangia Huduma hiyo kwa ushiriki wa pamoja na watumishi wa idara ya
afya.
Kauli hiyo imetolewa wakati mkuu huyo akipokea msaada wa vitanda Na
magodoro 18 kutoka katika kampuni ya taasisi za kifedha NMB Kanda ya magraribi Tabora
tawi la Kakonko lengo likiwa ni kuchangia kupunguza vifo vya mama Na
Mtoto katika wilaya ya Kakonko Mkoa wa Kigoma.
Ndagala amesema jitihada zinazofanywa na wadau pamoja na idara ya afya
zinaonyesha wazi kuwa vifo hivyo vitazidi kupungua siku hadi siku.
Aidha Mkuu huyo wa Wilaya ameipongeza Benk hiyo kwa msaada ulioutoa
katika hospital ya wilaya na kuwaomba watumishi na wananchi kuvilinda vitanda
Na magodoro yaliyotolewa kuweza kusaidia Wananchi Na Serikali kwa ujumla ili kuweza
kupunguza ukosefu wa vitanda.
KIMATAIFA
Wakuu wa Shirika la
ndege la Kenya, Kenya Airways, wanasema shirika hilo limepunguza kwa
kiwango kikubwa hasara ambayo shirika hilo limekuwa likipata, na kuibua
matumaini kwamba huenda shirika hilo likajikwamua.
Matokeo ya kifedha yaliyotangazwa na
Mkurugenzi wa kifedha wa shirika hilo Dick
Murianki yanaonesha shirika hilo lilipata hasara ya Sh bilioni 4.73 kabla
ya kulipa ushuru kipindi cha miezi sita hadi kufikia tarehe 30 Septemba.
Huku ni kuimarika kwa asilimia 60% ukilinganisha na hasara ya Sh
bilioni 11.86 ambayo shirika hilo lilipata kipindi sawa na hicho mwaka 2015.
Afisa mkuu mtendaji wa shirika hilo Mbuvi Ngunze amesema kuna matumaini
kwamba shirika hilo litajikwamua.
MICHEZO NA BURUDANI
Kocha
Joseph Omog amewataka wachezaji wake
kuamka na kuhakikisha wanatumia nafasi wanazozipata.
Simba
imekuwa moja ya timu zinazopoteza nafasi nyingi za kufunga mabao katika mechi
za Ligi Kuu Bara.
Omog raia wa Cameroon
ambaye mara kwa mara amekuwa akiwasisitiza wachezaji wake kuzitumia nafasi sasa
ameamua kuweka msisitizo.
Simba
inaongoza Ligi Kuu Bara ikiwa na pointi 29 baada ya kucheza mechi 11 huku Yanga
ikiwa na pointi 24 baada ya mechi 11 pia.
======= =======
=======
Katika ndondi,
Bondia
wa ngumi za kulipwa nchini, Abdallah
Pazi ‘Dulla Mbabe’ kesho
anatarajia kupanda ulingoni kuzichapa na Mchina, Chengbo Zheng
katika pambano lisilokuwa la ubingwa ambapo amefunguka kuwa kichapo
atakachompa hakitokuwa cha kawaida kwa upande wake kutokana na maandalizi
aliyoyafanya.
========== ========= ========
Nako barani uropa, Droo
ya Mechi za Robo Fainali ya EFL CUP,
Kombe la Ligi la England, imefanyika
jana mara baada ya Mechi ya mwisho ya Raundi ya 4 ambayo Man United iliwabwaga
Mabingwa Watetezi wa Kombe hili Man City
1-0 huko Old Trafford.
Katika Droo hiyo, Vigogo wote
wa Ligi Kuu England waliobakia
kwenye Mashindano haya wamepangwa kucheza Mechi zao Viwanja vya Nyumbani kwao
na hiyo ni faida kubwa kwao.
===== ======
======
Post a Comment