0

TAARIFA YA HABARI KUTOKA RADIO SENGEREMA


UHALIFU
Vijana  katika kijiji cha Nyanguku kilichopo kata ya Nyanguku wilaya ya Geita mkoani Geita, wametakiwa kufanya kazi kwa bidii ili kuepukana na vitendo vya uhalifu.
Taarifa na mwanahabari wetu  PETE KADASHI.
Hayo yamesemwa na viongozi wa kijiji hicho katika mkutano uliofanywa kwa ajili ya kubaini wezi wanaoiba mali za wakazi wengine.

Katika   Mkutano  huo  mwenyekiti wa kijiji cha Nyanguku pamoja na mtemi wa jeshi la jadi maarufu kama sungusungu wamesema, wizi unaofanyika ni ule unaofanywa majumbani wakati wa usiku.
Baadhi ya wanakijiji waliopata fursa ya kuzungumza na redio sengerema wamewaomba vijana kujishughulisha na kilimo ili kuondokana na uharifu kwa ajili ya usalama wa mali za wengine.
Mkutano huo uliofanyika katika kitongoji cha Bujingwa kijiji cha Nyanguku, umewabaini watu saba ambao  wadaiwa    kuwa na tabia ya kufanya uhalifu na  kupigwa faini ya shilingi 125,000  kwa kila mmoja .
Na, Mashamba /Mhariri   Twimanye            Chanzo: Mkutano.

MAENEO YA MAZIKO                         
Wananchi wilayani Sengerema Mkoani  Mkoani   wameitaka halmashauri  ya Wilaya ya  Sengerema kutenga    maeneo  mapya  ya maziko kutokana na maeneo  ya  awali   kujaa kwa muda mrefu bila kupatiwa ufumbuzi.
Wananchi    wamesema kujaa kwa sehemu  ya maziko kwa baadhi ya maeneo  hali hiyo  imesababisha adha kubwa pindi wanapokwenda kuhifadhi miili ya wapendwa wao ikiweko kukutana na mifupa ya binadamu waliozikwa zamani.

Hata hiyo   wamesema halmashauri ya sengerema ishughulikie suala hilo  mapema  ili kuondoa usumbufu kwa wananchi kuhangaika kutafuta mahali pa kuwahifadhi wapendwa wao.  

 Chanzo:Mahojiano.

UKATILI.
Jamii yatakiwa  kuwafichua   watu  wanaofanyia vitendo  vya  ukatili wa kijinsia     akinamama  ,wasichana na watoto  ili  kutokomeza vitendo hivyo hapa nchini.
Kauli hiyo imetolewa  na  Afisa  ufuatiliaji  na  tathimini   kutoka shirika la  Kivulini linalojihusisha na kutetea haki za wanawake na wasichana lililopo  Mkoani  Mwanza Bwn,Mathias Shimo  wakati akitoa mafunzo kwa wadau mbalimbali  dhidi ya kupinga ukatili  katika ukumbi wa mikutano Telecentre.
Kwa upande wao  baadhi ya wadau  waliopatiwa mafunzo  hayo   wamelishukuru  shirika hilo na kuahidi kwenda kuyafanyia kazi yote waliofundishwa katika maeneo yao ili kuhakikisha vitendo vya ukatili dhidi ya akinamama,wasichana na watoto vinapungua .
Shirika la Kivulini lenye makao yake makuu Mkoani Mwanza limezindua kampeni ijulikanayo kwa jina la TWAWEZA hivi karibuni  yenye lengo la kupinga ukatili wa kijinsia .

Na,Mhariri  Twimanye              Chanzo    Mahojioano.

UZINDUZI WA MADAWATI
Naibu waziri wa maliasili na utalii  Eng, Lwamo Makani amezindua ugawaji wa madawati elfu ishirini   yanayotolewa na wakala wa misitu nchini TFS  Mkoani    Mwanza .
Awali   kaimu mkurugenzi wa wakala wa misitu hapa nchini TFS  Bwn, Dosantos Silayo amesema kuwa wamefanikiwa kutengeneza madawati 12,115 sawa na asilimia 61 na kwamba  baadhi ya mashamba ya misitu  yalichelewa kuvunwa    na kusababisha kuchelewa kukamilisha asilimia 39 iliyobaki.
Akizindua ugawaji wa madawati hayo Eng. Makani amegawa madawati 2,580 kati ya madawati 12,115 yaliyotayari  kwa mikoa ya kanda ya ziwa ,Mwanza , Geita,Kagera, Simiyu na Mara huku kiasi kilichobaki  kikitazamiwa kutolewa kwa mikoa mingine hapa nchini.
Eng. Makani amesema kuwa kutekelezwa kwa mpango huo kumetokana na rasilimali mistu ambayo nayo inapaswa kutunzwa na wananchi wote.
Na,Meshack/Mhariri    Twimanye                 Chanzo   Uzinduzi.


KIMATAIFA.
Majaji wa kesi za uhalifu wa kivita mjini The Hague wamemhukumu kifungo cha miaka tisa gerezani aliyekuwa mwanamgambo wa itikadi kali aliyekiri kuyaharibu maeneo takatifu wakati wa mgogoro wa Mali mwaka wa 2012.
Hii ni  kesi ya kwanza   ambayo imelenga uharibifu wa turathi za kitamaduni.
Makundi ya kutetea haki za binaadamu na watalaamu wa kimataifa kuhusu masuala ya sheria wanasema   kuwa,  kesi dhidi ya Ahmad al-Faqi al-Mahdi katika Mahakama ya Kimataifa ya Jinai huenda ikasaidia kuzuia uharibifu wa aina hiyo unaoendelea kuigubika migogoro ya kimataifa bila kuchukuliwa hatua za kisheria.
Al-Mahdi ameelezea masikitiko yake kutokana na kuhusika kwake katika uharibifu wa nyumba 10 za makaburi na maeneo ya kidini mjini Timbuktu ambayo yalijengwa katika karne ya 14 nchini Mali.
Na,Mhariri  Twi manye   Chanzo                 Dw.

KIMAYTAIFA.
Taarifa  kutoka nchini  Marekani  zinaeleza  kuwa  Treni moja imegonga kituo cha reli kwenye mji wa Hoboken ulio jimbo la New Jersey nchini  humo.
Idara inayohusika na huduma za dharura jimba la New Jersey inaripoti kuwa watu watatu wameuawa na zaidi ya 100 kujeruhiwa .
Picha kwenye mitandao ya kijamii zinaonyesha uharibifu mkubwa  katika    treni hiyo   na kituo.
Kituo cha Hoboken kipo  umbali ya maili saba kutoka mji wa New York na watu wengi hukitumia kusafiri kwenda mtaa wa Manhattan.
Ben Fairclough ambaye alikuwa eneo hilo anasema   kuwa treni hiyo ilikuwa imetoka   kwenye njia yake. 
Na,  Mhariri   Twimanye  Chanzo        Dw.

             PATO
Pato    la Taifa limeendelea kukua kwa asilimia 7.9 katika kipindi cha mwezi Aprili hadi Juni  mwaka huu  ikilinganishwa na kasi ya asilimia 5.8 katika kipindi cha   mwaka  uliopita.

Takwimu hizo zimetolewa leo Jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mkuu wa  Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Dkt. Albina Chuwa alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu hali ya pato la Taifa kwa robo ya pili  kuanzia Aprili hadi Juni mwaka  huu.

Dkt Chuwa  amesema kuwa ukuaji wa pato la Taifa umetokana na shughuli za kiuchumi ikiwemo kilimo, mifugo, misitu na uvuvi ambapo shughuli  hizo zilikuwa kwa asilimia 3.2 ikilinganishwa na ukuaji wa asilimia 1.9 katika kipindi  cha  mwaka uliopita.

Kwa upande wa shughuli za uchumi za viwanda na ujenzi, Dkt. Chuwa amesema kumekuwa na ongezeko la asilimia 20.5 katika kipindi hicho ukilinganisha na ukuaji wa asilimia 11.2 mwaka 2015 katika shughuli za uchimbaji madini, mawe na kokoto.

Aidha katika shughuli za uzalishaji bidhaa na viwanda kumeongeza kwa asilimia 9.1 katika kipindi cha robo ya pili ya mwaka 2016 ukilinganisha na kasi ya asilimia 5.2 ya mwaka 2015.


Na, Mhariri   Twimanye   Chanzo           Michuzi


Post a Comment

 
Top