0
                    VYOO   BORA
Mkuu wa Wilaya ya  Sengerema   Mkoani      Mwanza Bwn,Emmanuel Kipole ametangaza kiama kwa wananchi ambao hawajajenga vyoo  vya kudumu  katika  makazi  yao.   
Katika mahojiano na Radio Sengerema   Bwn,Kipole amesema kuwa  kaya nyingi hazina vyoo  bora hasa katika maeneo ya mjini,  hali ambayo inapelekea wananchi kujisaidia ovyo na  amewagiza viongozi wote kuhakikisha kila kaya inajenga  choo.
Ameleza kuwa awali kulikuwa na ulegevu  wa  sheria juu ya   ufuatiliaji wa   suala la ujenzi wa vyoo  , lakini   kwa   sasa  watatembelea kaya moja hadi nyingine ili kuhakikisha kila kaya inakuwa na choo cha kudumu ili kuepuka magojwa ya milipuko.          
Hata hivyo  Bwn,Kipole amebainisha kuwa kwa yeyote atakae kaidi kujenga choo cha kudumu  hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake ikiwemo kupelekwa mahakamani kwani watu wachache wazembe hawawezi kusababisha Wilaya nzima  ya Sengerema  kukumbwa  na magonjwa ya milipuko.
                                 MTIHANI
Jumla ya watahiniwa 408,442 wa kidato cha nne wanatarajia kuanza mitihani ya kidato cha nne itakayoanza kesho, ikiwa ni idadi pungufu ya waliofanya mtihani huo mwaka jana.
Akizungumza na wanahabari leo Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani Tanzania Dk Charles Msonde amesema mwaka jana kulikuwa na watahiniwa  448,382 waliofanya mitihani huo.
Dk Msonde amesema maandalizi yote ya mitihani hiyo itakayomalizika Novemba 18, mwaka huu yameshakamilika.
Kawa wake Afisa Elimu Sekondari Wilayani Sengerema Mwl GODWINI BALONGO amewataka wanafunzi wote wa kidato cha Nne kutojihusisha na udanganyifu wa aina yoyote ili kuepuka kufutiwa matokeo.

                                     MAHAKAMANI.
Mtu   mmoja   amefikishwa   katika   mahakama   ya   wilaya   ya   sengerema  mkoani   mwanza   kwa   tuhuma   ya   ubakaji.
Taarifa zaidi na mwandishi wetu JOYCE ROLLINGSTONE alifika mahakamani hapo.
Akisoma  shitaka  hilo  mbele   ya   hakimu   wa  mahakama   hiyo   BI  MONIKA   NDYEKOBORA   mwendesha  mashitaka   wa  jeshi  la  polisi  INSPECTA  SLIVESTA   MWAISEJE  amemtaja   mshitakiwa   kuwa   ni  ALPHONCE   DEUSI   mwenye   umri   wa  miaka   18 mkazi   wa  NYAMLEGE   KATUNGURU.
INSPECTA  MWAISEJE  amesema  kuwa  mshitakiwa  anashitakiwa   kwa  kosa  la   kubaka   kinyume   na   kufungu  130  na  131   cha   kanuni  ya   adhabu  kuwa  mnamo  octoba  23  mwaka   huu  majira   ya  saa   3:00   usiku  eneo  la   katunguru  alimbaka  msichana  ambaye   jina   lake   limehifadhiwa  mwenye   umri  wa  miaka   16  mwanafunzi   wa   sekondari   kidato   cha  pili .
Hata  hivyo  mshitakiwa  amekana  kutenda  kosa  hilo,na yuko   nje   kwa  kutimiza   mashaliti   ya   dhamana hadi  NOVEMBA  14   mwaka   huu  kesi  hiyo  itakaposikilizwa   tena   mahakamani   hapo.
                                  MAZINGIRA
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amepiga marufuku uharibifu mkubwa wa mazingira unaendelea katika maeneo mbalimbali nchini ambao unaweza kusababisha nchi kugeuka jangwa.

Makamu wa Rais ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kufungua mkutano kimataifa unaohusu mabadiliko ya tabia ya nchi unaokutanisha wanasayansi, watafiti na wadau wa mazingira chini ya Usimamizi wa Kigoda cha mwalimu Julius Nyerere cha Mazingira na mabadiliko ya Tabia ya nchini katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Makamu wa Rais ameonya kuwa jukumu la kuhifadhi mazingira sio la Serikali peke yake bali ni kila mwananchi na wadau wa mazingira kwa ujumla, hivyo wananchi ni muhimu kwa umoja wao wakaongeza jitihada za kupanda miti katika maeneo yao ili kukabiliana na hali tete ya uhabifu wa mazingira nchini.

Makamu wa Rais ametahadharisha kuwa mabadiliko ya tabia ya nchi yameanza kuleta athari si kwa Tanzania na dunia kwa ujumla hivyo jitihada za makusudi zinahitajika ili kuhakikisha changamoto zinazojitokeza kwa sasa zinakabiliwa ipasavyo.

                                            AGIZO                                                                    
Mkuu wa wilaya ya uvinza mkoani Kigoma bw Mwanamvua Mlindiko amewataka viongozi wa serikali za vijiji wilayani humo kutowapokea wageni kutoka nchi jiarani wanaoingia katika vijiji hivyo kwa ajiri ya shughuli mbalimbali ikiwa ni pamoja na uvuvi kutokana na kuogopa kuhatarisha usalama.
Mkuu huyo wa wilaya ametoa agizo akiwa katika ziara yake kwenye vijiji vya mwambao wa ziwa Tanganyika ambavyo vimepakana na jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo baada ya taarifa za kuwepo kwa wageni na wahamiaji  wanaoingia na kuishi katika vijiji hivyo kinyume cha sheria hali ambayo imekuwa ikiongeza vitendo vya uharifu.
Kwa upande wao wananchi wamesema tatizo kubwa katika vijiji hivyo ni pamoja na kuingia wageni kutokana na serikali kutoajiri maafisa watendaji wa vijiji na kata hali iliyosababisha nafasi hizo kukaimiwa na watu wasiokuwa na uwezo nazo.
Mwenyekiti wa halmashauri wa wilaya ya Uvinza Jackson Mateso ameeleza kuwa shuguli za uvuvi zinazotegemewa na wananchi hao zimeendelea kuboreshwa licha ya kuwepo matatizo ya upungufu wa maafisa Uvuvi wilayani humo.
                                 KIMATAIFA          
Katibu mkuu wa Umoja wa mataifa Ban Ki-moon amempigia simu rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma ,akimtaka kutupilia mbali uamuzi wa serikali kujiondoa katika mahakama ya kimataifa kuhusu uhalifu wa kivita ICC.
Afisi ya bwana Ban imesema kuwa inathamini jukumu la taifa hilo katika kupigania haki na kwamba inatumai taifa hilo litaangazia upya uamuzi wake.
Afrika Kusini imesema mapema mwezi huu kwamba itajiondoa katika mahakama ya ICC kwa sababu ni kikwazo katika juhudi zake za kukuza amani barani Afrika.
Mwaka uliopita ,mahakama ya Afrika Kusini iliikosoa serikali kwa kukataa kumkamata rais wa Sudan Omar El bashir.
moon
Mataifa ya Burundi na Gambia tayari yametangaza kujiondoa katika mahakama hiyo.

                                 KIMATAIFA                   
Ripoti ya shirika la Umoja wa Mataifa linalowahudumia watoto-UNICEF inasema watoto milioni 300 kutoka kila pembe ya dunia wanaishi kwa kuvuta hewa chafu kupita kiasi.
Vijana,wake kwa waume katika eneo la kusini mwa Asia,Mashariki ya kati na Afrika sawa na wenzao wa Mashariki mwa Asia na eneo linalopakana na bahari ya Pacific ndio wanaoathirika vibaya sana na hali hiyo.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo,kila mtoto mmoja kati ya saba wa dunia hii anakabiliana hewa chafu,hewa ambayo imepindukia mara sita au zaidi kile kiwango kilichowekwa na shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO.
Duru nyengine za shirika la UNICEF zinasema jumla ya vijana bilioni mbili wa dunia wanavuta hewa ambayo si safi kuambatana na vipimo vya shirika la afya la Umoja wa Mataifa-WHO.
Chanzo cha hali hiyo ni moshi unaotoka ndani ya magari na wa viwandani,kuchomwa moto takataka za majumbani na vumbi.
                    MICHEZO NA BURUDANI

Bondia maarufu wa ngumi za kulipwa nchini, Thomas Mashali amefariki dunia usiku wa kuamkia leo October 31 2016 maeneo ya Kimara jijini Dar es salaam. 

Taarifa zinadai kuwa alishambuliwa na wananchi baada ya madai ya kuitiwa mwizi.

Taarifa kutoka kwa Promota wake, Siraji Kaike amesema watu aliokuwa anagombana nao walimwitia mwizi na wakawa wamemshambulia na kumtupa baadaye bodaboda waliokuwa wanamjua Thomas Mashali walimuokota na kumpeleka hospitali ambapo baadaye zilitolewa taarifa kuwa amefariki.

                    =======      =======   =======
HIVI karibuni, timu kadhaa zinazoshiriki Ligi ya Mpira wa Kikapu nchini Marekani (NBA), zilianza kuonyesha nia ya kumuwania Mtanzania Hasheem Thabeet Manka.

Timu hizo zilionyesha nia kutokana na maendeleo mazuri ya Hasheem katika timu yake ya Grand Rapid ambako ameendelea kuonyesha ubora wakati ikipambana katika D-League ya NBA.

Hasheem, aligoma kusaini kuzitumikia timu kubwa za mpira wa kikapu barani Ulaya katika nchi za Hispania, Ugiriki na kwingineko, akaamua kubaki D-League.


                        =====   ======    ======

BIASHARA
SERIKALI imesema, hakutakuwa na msamaha kwa mfanyabiashara au mzalishaji atakayeingiza sokoni bidhaa zisizothibitishwa ubora kwa sababu atakuwa amevunja sheria.
Akifungua maonesho ya bidhaa za wajasiriamali yaliyoandaliwa na Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO) mjini Bagamoyo mkoani Pwani , Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage amesema, wanaoingiza bidhaa sokoni bila kuzithibitisha ubora wanalihujumu soko.
Amesema kamwe serikali haiwezi kuwaonea haya wafanyabiashara wa aina hiyo, kwa sababu lengo lao ni ovu lenye dhamira ya kurudisha nyuma maendeleo ya nchi.
Mwijage amesema, Tanzania iko katika mchakato wa kuleta mabadiliko makubwa ya kiuchumi, kupitia uzalishaji wa viwandani, hivyo inahitaji wafanyabiashara na wazalishaji wa huduma na bidhaa wenye kuthamini ubora na sio kuzalisha ilimradi.
Amesema, huu ni wakati wa wajasiriamali nchini kuhakikisha wanafuata taratibu zinazotakiwa kuthibitisha ubora wa bidhaa wanazozizalisha, ili wajihakikishie mazingira salama ya kibiashara.
                                
                                 BIASHARA        
WIZARA ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji imesema kuwa mkakati wa Serikali ya Awamu ya Tano ni kuhakikisha mafuta ya kula yanazalishwa kutokana na mbegu zinazozalishwa nchini ili kuongeza ajira na kuokoa matumizi ya fedha za kigeni.


Hatua hiyo inatokana na Tanzania kuwa na hali ya hewa nzuri kwa uzalishaji mazao mbalimbali yanayozalisha mafuta, lakini imekuwa inaagiza kiasi cha tani  laki tatu na nusu (350,000)  za mafuta ghafi kila mwaka kutoka nje ya nchi, kwa fedha nyingi za kigeni.

Ofisa Biashara Mkuu, Idara ya Viwanda Vidogo na Biashara Ndogo kutoka Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Wilfred Kahwa amesema hayo juzi wakati alipowasilisha mada juu ya jitihada za serikali za uwekezaji kwenye sekta ya kilimo na viwanda.


Post a Comment

 
Top