0
            WAJASILIAMALI
MAKAMU wa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan ameelezea kukerwa na vitendovya rushwa na kuwataka wanawake wajasiriamali kufichua kila aina ya rushwa wanazoombwa na wenye mamlaka katika sekta ya biashara nchini.

Amesema hayo wakati akifungua kongamano la wajasiriamali wanawake lililoandaliwa na Mtandao wa Sauti ya Wajasiriamali Wanawake Tanzania (VOWET) na kuhudhuriwa na wanawake zaidi ya 500.

Amesema iwapo wanawake wakiwafichua waombaji wa rushwa wanaokwamisha harakati zao za kusonga mbele kibiashara, itaiwezesha serikali kuondoa kero hiyo.

Samia ameeleza baadhi ya wanawake wanaombwa rushwa za ngono na nyinginezo na hukaa kimya bila ya kulifikisha suala lao hilo kwa mamlaka husika ili wasaidiwe na kwamba kukaa kimya kumechangia kuendelea kuwepo kwa kero hiyo.

Amewahakikishia wanawake hao kuwa serikali itakuwa ikiwapa kipaumbele kwenye malipo ya fedha za zabuni ili waweze kusonga mbele zaidi

                                       CCM
MAKAMU Mwenyekiti wa CCM-Bara, Philip Mangula ameelezea kufurahishwa kwake kufukuzwa kwa wanachama 100 mkoani Mwanza kwa kubainika kukisaliti chama wakati wa uchaguzi mkuu uliopita.

Mangula amsema, wakati mikoa itaendelea kuchukua hatua, lakini pia kwa ngazi ya taifa hatua dhidi ya waliokisaliti chama zitaendelea kuchukuliwa, ikiwa ni pamoja na kuwatupilia mbali watakaojaribu kuomba nafasi za uongozi wakati wa uchaguzi wa Chama mwakani.

Mangula amewataka vijana nchini kote hasa wasomi, kuepuka kutumiwa vibaya na wanachama watakaokuwa wanasaka uongozi wakati wa uchaguzi mkuu wa CCM unaotarajiwa kufanyika mwakani, kwa kuwa kijana yeyote atakayekubali kutumiwa vibaya atakuwa amekisaliti chama.

                               MAHAFALI
Imeelezwa kuwa watoto wa kike wana nafasi kubwa ya kutimiza ndoto zao endapo wataamua kutoyakimbia masomo ya sayansi kutokana na sekta ya sayansi kuwa na wigo mpana wa fursa za kuajiriwa na kujiajiri ukilinganisha na sekta nyingine.

Hayo yameelezwa na wahitimu wa kidato cha nne 2016 katika Shule ya Mwilamvya Sekondari iliyopo wilayani Kasulu, wakati wa mahafali ya tisa ya kidato cha nne shuleni hapo.
  
Aidha wahitimu hao wamesema kuwa ili mtoto aweze kutimiza ndoto zake yampasa alelewe katika maadili tangu akiwa mdogo na kwamba kama wazazi nyumbani hawatawalea watoto katika maadili hawawezi kufanya miujiza wakiwa na walimu shuleni.

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Kasulu, Scarion Ruhula, ambaye alikuwa mgeni rasmi akimwakilisha Mkuu wa Wilaya kwenye mahafali hayo amewasihi wazazi na walimu wote kuwa wana jukumu la malezi ya watoto ili wakaishi vizuri katika jamii hata baada ya kumaliza masomo yao.

                                   NYUKI
MRADI wa ufugaji wa nyuki ambao upo katika moja ya Miradi ya Uhifadhi Mazingira Ziwa Victoria (LVEMP II) unakabiliwa na changamoto mbalimbali zilizosababisha kusuasua kwa mradi huo.

Akizungumza katika ziara maalumu ya kutembelea miradi ya Lvemp II wilayani Kwimba  Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Kwimba, Pendo Malabeja amesema mwamko wa jamii juu ya utekelezaji wa miradi hiyo wilayani kwake bado ni mdogo.

Malabeja amesema kuna mizinga 62 katika kata ya Kadashi, lakini ni mizinga 29 tu ndiyo inayofanya kazi.
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongela amemuomba Mkuu wa Wilaya ya Kwimba kuangalia upya miradi ya Lvemp II, kwani inaonekana haiko vizuri.
Aidha amemuagiza pia Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi wake wahakikishe kila ndani ya siku tatu za wiki wanatembelea miradi ya Lvemp II na kuiwekea usimamizi mzuri, kwani inaonekana fedha nyingi zinaliwa huku miradi hiyo ikisuasua.

                               KIMATAIFA                   
Wanajeshi wa Ethiopia wanaopigana na wapiganaji wa al-shabab nchini Somalia wameondoka katika kambi kubwa ya kijeshi huko Halgan katikatiki mwa jimbo la Hiran.
Walioshuhudia wanasema kuwa wapiganaji hao wa Jihad walichuka eneo hilo muda tu baada ya wanajeshi hao kuondoka.
Mamia ya watu wameanza kulitoroka eneo hilo wakihofia mashambulio ya kundi hilo.
Hii ni mara ya tatu mwezi huu ambapo wanajeshi wa Ethiopia wameondoka katika kambi muhimu nchini Somalia.
Imedaiwa kuwa huenda wanajeshi hao watahitajika kukabiliana na maandamano yanayoendelea nchini mwao.
                              KIMATAIFA                   
Mashambilizi makali ya angani yamelejea katika mji wa Aleppo baada ya muda wa siku tatu wa usitishwaji mapigano uliokuwa umetangazwa na Urusi kukamilika.

Mashambulio ya angani yameripotiwa katika maeneo kadhaa ikiwa ni pamoja na yale yanayokaribiana na maeneo ya Sheikh Saeed na Salah el-Deen.

Maeneo mengine yanayoshikiliwa na waasi pia yanalengwa katika mashambulio hayo japo haijabainika iwapo yanatekelezwa na ndege za Urusi au Syria.

Umoja wa Mataifa umesema haukufanikiwa kumuondoa mtu yeyote katika maeneo yanayodhibitiwa na waasi ambayo yamezingirwa wakati wa kipindi cha usitishwaji mapigano kwa sababu maafisa wake hawakuhakikishiwa usalama wa kuendeleza shughuli hiyo.

MAKAMU Mwenyekiti wa CCM-Bara, ameelezea kufurahishwa kwake kufukuzwa kwa wanachama 100 mkoani Mwanza.
             ========    =========     =========

Imeelezwa kuwa watoto wa kike wana nafasi kubwa ya kutimiza ndoto zao endapo wataamua kutoyakimbia masomo ya sayansi.
                  ===========    ==========

                     Na katika duru za kimataifa,
Mashambilizi makali ya angani yamelejea katika mji wa Aleppo baada ya muda wa siku tatu wa usitishwaji mapigano kukamilika.
         ===========      ============     ========


Post a Comment

 
Top