0
                                  MIKUTANO

Wakazi  wa kitongoji cha kanyamwanza  kata ya mwabaruhi wilayani sengerema wametakiwa kujitokeza kwenye mikutano  ya kijiji ambayo huitishwa na viongozi kwa ajili ya maendeleo ya maeneo yao.
Hayo yamesemwa na mwenyekiti wa kitongoji cha kanyamwanza Bw. INNOSENT SEGEREDI ambapo amesema wananchi wamekuwa hawajitokezi kwenye mikutano ya kijiji ili kusomewa mapato na matumizi na kujadili shughuli  za maendeleo.
Kwa upande wao wananchi wa eneo hilo wamekiri kutohudhuria mikutano hiyo hivyo wamewataka viongozi wa kijiji hicho kuongeza hamasa ya kualika wananchi ikiwa ni pamoja na kujiwekea sh
                                     
                                      TUKIO

Mtu mmoja  ambaye hajafahamika mara moja jina lake wala makazi yake  amekamatwa na Jeshi la polisi  wilayani Sengerema baada ya kufanya kitendo cha kujizulu mwili kwa kujikata tumbo lake kwa kutumia  kisu.
Mtu  huyo aliyekamatwa na vyombo vya usalama ametiwa nguvuni  akiwa katika eneo la kituo cha Habari na mawasiliano Sengerema Telecentre.
Mpaka sasa haijafahamika  chanzo cha kutaka kufanya kitendo hicho  ingawa mashuhuda wa tukio  waliomuona wakati anafika kituoni hapo  wanasema awali wakati anafika  eneo hilo alikuwa anafukuzwa na wananchi.
Mashuhuda hao wameeleza kuwa tukio hilo ni la ajabu  na la kusikitisha kutokana na kitendo hicho cha kujikata tumbo lake hali iliyopelekea utumbo kutokeza kwa nje.
Kufuatia Tukio hilo, Radio Sengerema inaendelea  kuwatafuta viongozi wenye mamlaka ili kupata tamko la serikali kuhusiana na tukio hilo.

                       USALAMA  BARABARANI.
Kamanda  Mkuu wa  kitengo cha usalama barabarani wilayani sengerema mkoani Mwanza, Insipecta Hamis Wembo, amewaasa madereva kuvaa sare zao ili kuwatofautisha kati yao na abiria.
Insipecta Wembo ameyasema hayo wakati akizungumza na kituo hiki kwa njia ya simu kuwa, madereva na makondakta wote  wa magari madogo na mabasi makubwa wanatakiwa kuvaa sare ili kuwatenganisha wao na abiria.
Inspekta Wembo ameeleza kuna mtindo kwa baadhi ya madereva kuvaa sare pindi wanapomuona askari wa usalama barabarani mbele yao kitu ambacho hakikubariki na wanapaswa kuvaa muda wote wa safari  na wanapaswa kuwa wasafi.
Maelezo haya yamekuja kufuatia radio sengerema kufanya uchunguzi na kubaini madereva wanaofanya safari zao sengerema kuelekea Kamanga, na Sengerema kuelekea Buchosa wengi wao wamekuwa hawana desturi ya kuvaa sare hizo na hivyo kushindwa kuwatofautisha wawapo kituo cha mabasi.
                                
                               UPANDAJI MITI

Serikali kupitia ofisi  ya makamu wa rais imesema kuanzia mwakani kila mwanafunzi anaeanza darasa la kwanza na kidato cha kwanza atatakiwa kwenda na mti atakaouotesha na kutunza kipindi chote atakapokuwa shuleni.
Kauli hiyo imetolewa na waziri wa nchi ofsi ya makamu wa rais muungano na mazingira January Makamba mara baadaya kutembelea na kushiriki zoezi la upandaji miti katika shule ya msingi Mlandege wilayani Iringa na kusema kuwa kwa kufanya hivyo nchi itakuwa na miti ya kutosha.
Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Irinaga Amina Masenza amesema atasimamia zoezi pamoja na kuwatoa wakulima wanao lima karibu na vyanzo vya maji huku wanafunzi walioshiriki katika kupanda miti na waziri Makamba  amewahimiza kuitunza miti hiyo.
                                    TASAF
 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Utumishi na Utawala Bora  Angellah Kairuki amesema  jumla ya kaya 5457 zitaondolewa katika mpango wa kukomboa kaya masikini kutokana na kutokuwa na sifa za kupata msaada huo.
Akizungumza mbele ya watendaji na wasimamizi wa halmashauri Kairuki amesema idadi hiyo imesababisha upotevu wa fedha nyingi ambazo hazikuwafikia walengwa wa mradi huo.
Ameongeza kuwa kaya hizo hewa hazitapewa fedha hizo kwa awamu ijayo ya nane   na badala yake kaya stahiki ambazo ni asilimia 76 zitaingia kwenye mpango huo.
Awali akisoma taarifa ya utekelezaji wa mradi huo Mratibu wa TASAF Esterine Sephania amesema licha ya kuwepo kwa changamoto kadha wa kadha mradi huo umesaidia kubadili hali za uchumi wa kaya masikini.
                                      KIMATAIFA                  
Wagombea wa kiti cha urais nchini Marekani Hillary Clinton na Donald Trump wamelumbana vikali katika mdahalo wa tatu na wa mwisho ikiwa zimebaki siku chache kabla ya uchaguzi mkuu kufanyika.
Wagombea wote wawili wameelezea masuala mbalimbali ikiwemo uhamiaji, uchumi, majaji wa mahakama kuu, mizozo ya kimataifa, na haki za wachache.
Mada nyingine zilizogusiwa ni utoaji mimba, matumizi ya serikali, sheria ya umiliki wa silaha na mengine mengi.
Mgombea wa chama cha Republican Donald Trump ameonyesha dalili za kuyakataa matokeo ikiwa atashindwa akisema kura zinaweza kuibiwa.
Kwa mujibu wa Utafiti uliofanywa na kituo cha televisheni cha CNN, asilimia 52 ya watazamaji wamesema Clinton kutoka chama cha Democratic ameshinda mdahalo huo huku asilimia 39 wakisema ni Trump.
                              KIMATAIFA                    
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-moon ameelezea matumaini kwamba makubaliano yaliofikiwa katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ya kuchelewesha uchaguzi hadi mwaka 2018 yatasaidia kuimarisha haki za binaadamu na kusababisha kuwepo kwa uchaguzi wa kuaminika.
Taarifa iliyotolewa na Umoja wa Maatifa imesema Ban anazingatia makubaliano hayo na anatumai kwamba utekelezaji wake utachangia kuweka mazingira ya kuheshimiwa kwa haki za binaadamu na uhuru ambavyo ni muhimu kwa mjadala wa kisiasa na uchaguzi unaoaminika.
Katibu Mkuu huyo ameitaka serikali ya Kongo kuendelea na hatua za kujenga imani na upinzani, hasa kwa kuwaachia wafungwa wa kisiasa na kuheshimu haki ya mikusanyiko ya amani.
Maandamano ya kumpinga Rais Joseph Kabila mwezi uliopita yaligeuka kuwa machafuko na watu wapatao 49 waliuawa.
                MICHEZO NA BURUDANI
Ligi kuu Tanzania bara imeendelea tena leo  huku vinara wa ligi kuu  Stimu ya simba wakiibuka kidedea kwa kuwafunga Mbao Fc kwa goli 1-0 katika uwanja wa uhuru jijini Dar es salaam.
Mtanange huo ulianza kwa kushambuliana kwa zamu huku simba sport wakionekana kukamia kupata magoli ya mapema, lakini mpka dakika za lala salama wanafanikiwa kufunga goli hilo.

                    =======      =======   =======
Meneja wa Manchester City Pepe Guardiola anasema kuwa hatobadili filisofia yake licha ya klabu yake kufungwa 4-0 na Barcelona katika uwanja wa Nou camp.
Lionel Messi alifunga hat-trick dhidi ya Manchester City iliokuwa na safu ya ulinzi ilio legea huku kipa Claudio Bravo akipewa kadi nyekundu kwa kushika mpira.
Barcelona inaongoza kundi C na pointi tisa ,ikiwa mbele kwa pointi tano.

                          =====   ======    ======


Post a Comment

 
Top