SHERIA MKONONI

Baadhi
ya wananchi wamesema kuwa wamefikia hatua hiyo ya kujichukulia sheria mkononi
kutokana na marehemu huyo kukithili
kutenda vitendo vya wizi.
Akithibitisha kutokea kwa tukio
hilo mwenyekiti wa mtaa huo Bw. Magulutatu
Juma amemtaja mtu aliyeuawa kuwa ni Simon Phillipo mwenye umri wa miaka 50.
Hata
hivyo Bw. Juma amesema kuwa jeshi la polisi mkoani Geita limefika eneo la tukio
na kufanikiwa kuwakamata wananchi watano ili kusaidia upelezi wa tukio hilo.
KUSIMAMISHWA
WAZIRI MKUU Kassim
Majaliwa amemsimamisha kazi Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Lindi Mhandisi Adam
Alexander kwa kosa la matumizi mabaya ya ofisi pamoja na kushindwa
kusimamia ujenzi wa kituo cha kuzalisha maji katika Manispaa ya Lindi.
Waziri Mkuu amemkabidhi Mhandisi huyo kwa
Kamanda wa TAKUKURU Mkoa wa Lindi, Bw. Stephen Chami na
kumuelekeza afanye uchunguzi zaidi juu ya suala hilo.
Waziri Mkuu ametoa agizo hilo leo wakati alipotembelea mradi wa maji wa Ng'apa
ambapo ameagiza nafasi hiyo ikaimiwe na Mkurugenzi Msaidizi wa mamlaka
hiyo, Mhandisi Idrisa Sengulo.
Mhandisi huyo anakabiliwa na tuhuma mbalimbali
ikiwemo matumizi mabaya ya fedha za ofisi pamoja na kupokea mshahara bila kulipa kodi ya mapato ya mshahara (PAYE),
kujilipa kiwango kikubwa cha posho pamoja na kusafiri kwa muda mrefu.
NEC
Tume Ya Taifa Ya
Uchaguzi (Nec) inaendelea kutekeleza mkakati Wa Kutoa Elimu Ya Mpiga Kura Kwa
Wananchi Ili Kuimarisha Demokrasia Nchini.
Mwenyekiti Wa Tume
Hiyo Jaji Mstaafu Damian Lubuva ametoa Wito Kwa Wananchi Kuendelean
Kutoa Ushirikiano Wao Kwa NEC Ili Kufanikisha Mkakati Huo
Kwa Upande Wake
Mkurugenzi Wa Uchaguzi Wa Tume Ya Taifa Ya Uchaguzi Bw. Kailima Ramadhani
amewataka Wananchi Kuhakikisha Elimu Ya Mpiga Kura Inawafikia na kuielewa ili
waweze kutambua demokrasia.
Mkakati Wa Kutoa Elimu Ya Mpiga Kura Ni Utekelezaji
Wa Kifungu Cha 4 (C) Cha Sheria Ya Uchaguzi Ya Mwaka 1985 Inayoitaka Tume Ya
Taifa Ya Uchaguzi Kutoa Elimu Hiyo, Kusimamia Na Kuratibu Asasi Na Taasisi
Zinazotaka Kutoa Elimu Ya Mpiga Kura.
MKATABA.
Ubalozi wa Norway nchini
umesaini mkataba wenye thamani ya Tsh. Bilioni 10.6 na Umoja wa Mataifa (UN)
kupitia Mpango wa Misaada ya Maendeleo (UNDAP 2) kwa ajili ya kuwasaidia
wakimbizi waliopo hapa nchini.
Akizungumza katika hafla ya
utilianaji saini mkataba huo, Balozi wa Norway nchini, Hanne-Marie Kaarstad amesema
pesa ambazo wamezitoa zinalenga zaidi kuwasaidia wakimbizi waliopo mkoani
Kigoma ili waweze kuwa na shughuli za kuwasaidia na hasa kwa wanawake na
watoto.
Nae Mratibu Mkuu wa Mashirika
ya Umoja wa Mataifa (UN), Alvaro Rodriguez amesema ni jambo zuri kuona Norway inaendeleza
ushirikiano na Tanzania na wao wamejipanga kuhakikisha wakimbizi wanaokusudiwa
kunufaika na pesa hizo zinawafikia na kufanya kazi ambayo zimepangiwa
kufanyika.
UTALII
Waziri wa Maliasili na
Utalii, Profesa Jumanne Maghembe amesema tabia ya udokozi ni
miongoni mwa sababu ambazo zinazowafanya wenye hoteli wapende kuajiri wageni
badala ya watanzania.
Mwandishi wetu SARAH CHARLES anataarifa zaidi.
Akizungumza na wafanyakazi
wa Chuo cha Taifa cha Utalii, Maghembe amesema
kazi za hoteli zinahitaji watu waaminifu na wanaojituma.
Profesa Maghembe ametoa
wito kwa uongozi wa chuo hicho kufundisha uaminifu katika kazi ili wageni
waweze kukaa kwa amani.
Biashara zimefungwa Kinshasa katika
Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo na hakuna magari barabarani kufuatia
wito wa upinzani kuwa watu wakae ndani katika kushinikiza uchaguzi mkuu nchini
ufanyike Novemba na Rais Kabila ajiuzulu.
Mwandishi wa BBC aliyeko mjini Kinshasa
anasema vikosi vya usalama vimeizingira nyumba ya mpinzani mkuu wa rais Kabila, Etienne Tshisekedi, ambaye ndiye anaongoza wito wa uchaguzi
ufanyike Novemba mwaka huu.
Chama chake kimeonya kuwa rais Kabila
atakuwa anatekeleza 'uhaini wa hali ya juu' iwapo uchaguzi utacheleweshwa.
Katiba inamzuia Kabila
kuwania muhula wa tatu, na upinzani unatuhumu kuwa serikali inataka
kuchelewesha uhaguzi huo ili Kabila
asalie madarakani.
Chama tawala na kimoja cha upinzani vimependekeza kuchelewesha uchaguzi
wa urais hadi mwezi Aprili 2018.
Watu kadhaa wameuawa mjini Kinshasa mwezi uliopita katika
maandamano ya kumtaka rais Kabila
aondoke madarakani
KIMATAIFA
Ethiopia
imedhibiti usafiri wa wanadiplomasia wa kigeni na kupiga marufuku mikutano na
upinzani ulioko nje ya nchi kama sehemu ya hali ya hatari iliotangazwa nchini
humo.
Wanadiplomasia
hawaruhusiwi tena kusafiri zaidi ya kilomita 40 nje ya mji mkuu wa Ethiopia Addis Ababa.
Vikwazo
hivyo vipya vinahusisha pia kile kinachotajwa kuwa "ukanda mwekundu"
wa maili 30 kwenye mipaka ya nchi hiyo, ambapo ni haramu kubeba silaha, na pia
amri ya masaa 12 ya kutotembea usiku katika maeneo ya viwanda na karibu na
majengo ya serikali.
Hatua
hizo zimeanzishwa kufuatia wimbi la maandamano ya kuipinga serikali.
MICHEZO NA BURUDANI
Mwanasoka wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana
Ally Samatta anayechezea KRC Genk ya Ubelgiji amesema kwamba kuingizwa
kwenye kinyang'aniyo cha tuzo ya Mwanasoka Bora Afrika ni heshima kuu kwa nchi
yake.
Samatta, amesema amefurahi juu ya uteuzi huo, kwani anajiona anaendelea
kuiwakilisha vyema nchi yake katika soka.
Mwanasoka Bora wa Afrika pamoja na kipa Mganda, Dennis Onyango anayechezea Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini na
kiungo Mkenya, Victor Wanyama
anayechezea Tottenham Hotspur ya England.
Orodha hiyo ina Waalgeria watatu; mshambuliaji wa mabingwa wa England, Riyad Mahrez, Islam Slimani wa
Leicester City na El Arabi Hillel
Soudani wa Dinamo Zagreb.
======= ======= =======
Kwa
mujibu wa mwandaaji wa pambano hilo Jay
Msangi, mshindi wa pambano hilo atajinyakulia Mkanda wa ubingwa, huku pia
kukiwa na mapambano mengine mengi ya utangulizi ambayo yatawakutanisha mabondia
kutoka Tanzania na nje ya Tanzania.
Jay Msangi amesema kwa sasa wataandaa mapambano
mengi ya kimataifa kwa mabondia wa Tanzania kwa lengo la kuwandaa kufuzu
mashindano ya Olimpiki nchini Japan.
BIASHARA
KAMPUNI ya Uwekezaji ya TCCIA imejipanga kuwekeza katika
sekta ya viwanda vya kusindika mazao ya kilimo, ili kuchangia kukuza uchumi wa
taifa na ajira.
Akifungua mkutano mkuu wa 11 wa kampuni hiyo Dar es
Salaam Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi,
Aloys Mwamanga, amesema wamejipanga kuanzisha viwanda vya usindikaji wa
mazao ya kilimo.
Amesema kampuni inaunga mkono kwa dhati dhamira ya
Serikali ya kuwekeza katika sekta ya viwanda na hasa viwanda vya kusindika
mazao.
Mwenyekiti huyo ameongeza kuwa kampuni imepanga kuwekeza
pia katika dhamana za Serikali, benki, uanzishaji wa taasisi za fedha
zinazohusika na mitaji midogo, ujenzi wa jengo la ofisi na maghala ya kuhifadhi
bidhaa.
BIASHARA
Wito umetolewa kwa jamii ili waweze kuwa na
maisha bora wawe na shughuli za halali za kufanya zitakazo waingizia kipato,ili
wasiwe tegemezi katika familia zao na jamii kwa ujumla.
Kauli hiyo imetolewa na Jaggy Singh
ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa ushirika ( FGBMFI) wa Kimataifa wa wafanyabiashara
Wakristo,ambapo amewataka watu kufanya shughuli zao katika misingi iliyo halali
,katika uadilifu na waepuke udanganyifu.
Sigh
amesisitiza kuwa lengo kuu la mkutano ni kuwaleta wafayabiashara pamoja,
kubadilishana mawazo na changamoto wanazopitia,kuonyesha umuhimu wa kuishi
maisha ya uhalisia na kufanya kazi kwa bidii zaidi,ambapo amewataka kuepuka
udanganyifu kwa kutokulipa kodi ,wafuate utaratibu na sheria za nchi.
Post a Comment