0

TAARIFA YA HABARI KUTOKA RADIO SENGEREMA FM

RAIS   KUSHIRIKI  IBADA      
Rais Dkt. John Pombe Magufuli, leo ameungana na Waumini wa Kanisa la Anglikana la Mtakatifu Albano lililopo Posta Jijini Dar es Salaam kusali ibada ya Jumapili ya kuadhimisha Siku ya Bwana ya 19 baada ya Pentekoste.


Akizungumza na Waumini wa Kanisa hilo baada ya kumalizika kwa Ibada, Rais Magufuli aliyeongozana na Mkewe Mama Janeth Magufuli amewashukuru Viongozi na Waumini wa Kanisa la Anglikana na Madhehebu mengine ya Dini hapa nchini kwa kuendelea kuliombea Taifa na kudumisha amani na utulivu.

Dkt. Magufuli amesisitiza kuwa Viongozi wa Dini wanafanya kazi kubwa na muhimu katika Taifa na kwamba Watanzania wote bila kujali dini zao, itikadi za kisiasa, makundi na kanda zao wana wajibu wa kuungana na Viongozi hao ili nia hiyo njema iendelee kufanikiwa.


Kwa upande wake Padre Jackson Sostenes aliyeongoza Ibada hiyo amemshukuru Rais Magufuli kwa kuungana na waumini wa Kanisa hilo katika  ibada ya Jumapili na ameahidi kuwa Viongozi na Waumini wa Kanisa hilo wataendelea kumuombea na kuliombea Taifa.

Katika Ibada hiyo Rais Magufuli ametoa Shilingi Milioni moja  kuchangia vikundi vya kwaya vya kanisa hilo.

 Na, Mhariri   Twimanye     Chanzo         Mpekuzi.
VITHIBITI    MWENDO
Wakazi wa kijiji cha Tabaruka Wilayani Sengerema  wameitaka  serikali  kuchukua jitihada    za makusudi   kuweka vithibiti  mwendo  katika  barabara itokayo  mjini Sengerema  hadi   Busisi   ili  kunusuru  vifo vya watoto vinavyosababishwa na  ajali  za   barabarani.    
Matamshi ya wakazi  hao   yanakuja  siku chache  baada ya  wanafunzi  wawili  wa shule  ya msingi  Tabaruka   kupoteza maisha kwa kugongwa  na  gari . 
Katika   mahojiano  na  Radio  Sengerema    wananchi      wamedai  kuwa  ukosefu wa vithibiti mwendo ni chanzo  kinachosababisha   ajali za barabara,  na serikali   kubaki   kuwatupia lawama  wakazi  wa eneo hilo  pekee  badala ya madereva.       
Kwa  upande wake   Mkuu wa usalama barabarani   Wilayani  Sengerema  Inspecta  Hamis  Wembo  amewaomba wazazi kuwaangalia  watoto  pindi  wanapovuka barabara  ili kuepuka  ajali hizo wakati    serikali   ikilitafutia ufumbuzi  suala   la kuweka  vithibiti  mwendo katika   barabara hiyo.    
Aidha  ukosefu  wa vithibiti mwendo  katika  kijiji cha Tabaruka  limekuwa ni tatizo la  muda mrefu bila kupatiwa ufumbuzi.    .


MAFUNZO.            
Wananchi  wilayani   Sengerema mkoani Mwanza wametakiwa kujikita   katika       mafunzo   ya   teknolojia, ufundi   pamoja na ujasiliamali   ili waweze kujikwamua kimaisha.
Kauli hiyo   imetolewa   na msimamizi wa  taasisi  ya Elabs inayojishughulisha  na shughuli za kijamii ikiwemo kuwawezesha vijana Wilayani  Sengerema  Bi. Jackline Dismas katika mkutano  wa  kuwahamasisha vijana kujiunga   na   mafunzo  hayo    uliofanyika kata ya Sima.
Bi.Jacline,     amesema hatua ya kuitisha mkutano  huo imekuja baada ya wananchi kuoomba  yawepo mafunzo  hayo  ili waondokane na  umasikini.
Aidha msimamizi wa taasisi hiyo  amebainisha kuwa wameamua kuhamasisha suala hilo kutokana na wananchi wilayani  hapa kuwa na mwitikio mkubwa wa kujitokeza kwenye mafunzo hayo.

Veronica   /Mhariri   Twimanye   Chanzo  Mkutano .       









KUMWENZI BABA WA TAIFA   

Katika  kuelekea  kuadhimisha   kumbukumbu   ya   miaka 17  ya  kifo cha Baba wa Taifa  hayati  Mwalimu Julius   Kambarage  Nyerere  Oktoba  14 mwaka huu ,viongozi wa vyama vya Siasa wametakiwa kuiga kwa vitendo uzalendo     aliokuwa nao Baba wa Taifa     enzi za uhai wake,  ili kuliwezesha Taifa kupiga hatua kimaendeleo.

Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Bw. Kailima Ramadhani  mara baada  kutembelea Kaburi na Makumbusho ya Baba wa Taifa eneo la Mwitongo wilayani Butiama.

Amesema kuwa kumbukumbu za Baba wa Taifa zilizohifadhiwa vizuri katika makumbusho hiyo zina mambo mengi ya kujifunza ambayo wanasiasa wanatakiwa kuyafanya kwa  vitendo hasa  uzalendo kwa nchi, uvumilivu, upendo  na moyo wa kujitoa kwa dhati kuwatumikia wananchi.


Ameeleza kuwa maisha aliyoishi Baba wa Taifa ni mfano wa kuigwa na viongozi na watanzania wote hasa pale alipojitofautisha na viongozi wengi wa Bara la Afrika alipoepuka tamaa ya madaraka na mali kwa  manufaa ya taifa.

 

Aidha  Bw. Kailima amebainisha kuwa  NEC itaendelea  kumuemzi Baba wa Taifa kwa yale aliyoyafanya na kuyasimamia kwa manufaa ya taifa huku akitoa wito kwa  viongozi wa vyama vya Siasa wawe na kiasi na waridhike na vile walivyonavyo.



Na, Mhariri   Twimanye  chanzo   Mpekuzi.

MAHAFARI.                                                                          
Shule  Msingi Sayuni iliyopo katika kata Mwabaluhi  Wilayani   Sengerema   inakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa  uzio, pamoja  na    vifaa vya kufundishia  kwa muda mrefu bila kupatiwa ufumbuzi.
Changamoto  hizo  zimebainika  katika   risala  ya wahitimu iliyosomwa  na  Shallon Sinai kwa niaba ya wahitimu wote     mbele ya mgeni rasmi Mchungaji   Joakimu Masama.  
Naye mgeni rasmi Mchungaji Masama akijibu risala ya wahitimu, amesema kuwa changamoto hizo ataziwasilisha katika kamati ya shule hiyo ili zitatuliwe.      
Kwa upande wake mwalimu mkuu wa shule ya msingi SayuniSaimon Manoni amesema kuwa shule hiyo ilianzishwa mwaka 2009  ikiwa na walimu  wawili  pekee,  ambapo  kwa sasa    ina jumla ya walimu 14  wakiwemo  wakike sita na wakiume wanane.
Na,Mhoja/Arafa/Mhariri   Twimanye  Chanzo Mahafari.

 25/09/2016                       KIMATAIFA.
Kiongozi wa kundi la waasi la Sudan kusini , Riek Machar, ametoa wito wa  kuhimiza  vuguvugu la kivita la kuipinga serikali ya nchi hiyo.
Awali bwana Machar alikuwa amerudi katika mji mkuu wa Juba kama sehemu ya utekelezwaji wa mkataba wa amani lakini amelazimika   kwenda tena uhamishoni   Julai  mwaka huu, baada ya kuzuka mapigano yaliyowauwa mamia ya watu .
Taarifa hii imetolewa baada ya Bwana  Machar  kukutana na wanachama wa kundi lake  huko    nchi jirani ya Sudan.
Hata hivyo baadhi ya viongozi wa juu wa kundi lake hawamuungi mkono tena.
Mmoja wao ni Taban Deng ambae amejiunga na serikali amerithishwa wadhifa wa makamu wa rais nafasi iliyokuwa ya Bwana Machar.

Na,  Mhariri  Twimanye   Chanzo         BBC.







KIMATAIFA.
Umoja wa   ulaya umesema mashambulizi yanayoendelea dhidi ya raia katika mji wa Aleppo kaskazini mwa Syria ni ukiukwaji mkubwa wa sheria za kimataifa juu ya ubinaadamu, ukitoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kuzidisha juhudi za kurejesha amani nchini humo.
Mkuu wa sera za nje wa Umoja wa Ulaya, Federica Mogherini, na Kamishina wa Masuala ya Kibinaadamu, Christos Stylianides, wamesema mashambulizi dhidi ya raia wasio na hatia ni jambo lisilokubalika .
Marekani inadai msafara huo ulishambuliwa na ndege za kivita za Urusi ambayo inaendesha operesheni ya kijeshi ikiuunga mkono utawala wa Rais Bashar al-Assad.
Maafisa wa Umoja wa Mataifa wanasema karibu raia milioni mbili wamekosa huduma ya maji katika mji huo wa kaskazini baada ya mashambulizi ya mabomu yaliyofanywa na vikosi vya serikali kuharibu mtambo wa kusukuma maji.
Wakati huo huo, Uingereza, Ufaransa na Marekani zimetoa wito wa kuitishwa kwa kikao cha haraka cha dharura cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kujadili juu ya kuendelea kwa mashambulizi katika mji wa Aleppo.
Na,  Mhariri   Twimanye   Chanzo                      DW.

NA HUO NDIO MWISHO WA TAARIFA YA HABARI  KUTOKA RADIO SENGEREMA FM.






Post a Comment

 
Top