TAARIFA YA HABARIKUTOKA RADIO SENGEREMA FM
Mahakama ya Wilaya ya Mpanda
mkoani Katavi imemhukumu Ally Rashid , kifungo cha miaka 30 jela baada ya
kupatikana na hatia ya kumlawiti msichana mwenye umri wa miaka 25, katika Mtaa
wa Kotazi, Manispaa ya Mpanda..
Hukumu hiyo imetolewa na Hakimu wa mahakama hiyo, Chiganga Ntengwa baada ya kuridhika na ushahidi uliotolewa na
upande wa mashitaka pasipo kutia shaka, ukiongozwa na Mwanasheria wa Serikali
wa Mkoa wa Katavi, Jamila Mziray.
Awali Mwendesha Mashtaka Mziray
alidai mahakamani hapo kuwa mshtakiwa huyo alitenda kosa hilo Juni 17, mwaka
huu, saa 2:00 usiku katika makaburi ya Kashaulili
yaliyoko katika Mtaa wa Kotazi, Manispaa ya Mpanda.
Inadaiwa kuwa mshtakiwa kabla ya kutenda kosa hilo alimfuata
msichana huyo ambaye alikuwa ameibiwa vitu vyake vya ndani ya nyumba na kuwa ana uwezo wa kumsaidia kuvipata vitu
vyote alivyoibiwa.
Mziray amedai kuwa baada ya msichana huyo kuahidiwa na mshtakiwa
kuwa vitu vyake alivyoibiwa vitapatikana alimlipa mshtakiwa Shilingi elfu thelathini ili akamwoneshe vitu vyake alivyoibiwa.
Ilidaiwa mahakamani hapo kuwa siku hiyo ya tukio mshtakiwa
alimpigia simu msichana huyo saa 2:00 usiku akimtaka waonane ili akamwonesha
vitu vyake vilivyoibiwa.
Mziray ameeleza mshtakiwa
alikwenda nyumbani kwa msichana huyo na wakaongozana hadi kwenye makaburi ya
Kashaulili ambako alidai ndiko vilipo vitu vilivyoibwa lakini ghafla mshtakiwa
alimpiga ngwala msichana huyo na kumbaka na kumlawiti huku akimtishia
maisha iwapo akijaribu kupiga kelele.
TANESCO
Shirika
la Umeme Nchini Tanzania, TANESCO,
limewatahadharisha wananchi mkoani Kagera kutogusa nyaya za umeme kwenye
nyumba zilizoanguka au kupata athari kubwa kutokana na tetemeko la ardhi
lililoukumba mkoa wa Kagera wakati wafanyakazi wa Shirika hilo wakiendelea na
zoezi la kuondoa nyaya hizo.
Wito
huo umetolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika hilo, Mhandisi Felchesmi
Mramba, wakati alipomtembelea Mkuu wa Mkoa wa Kagera,
Meja Jenerali mstaafu Salum Kijuu, ili
kumpa pole kutokana na maafa haayo.
Sambamba
na wito huo, Mkurugenzi huyo pia amemuhakikishia Mkuu huyo wa Mkoa kuwa
upatikanaji wa umeme mkoani humo utakuwepo bila shaka yoyote isipokuwa kwenye
maeneo ambayo nyumba zimeathirika vibaya ili kuepusha athari zozote zinazoweza
kutokea kutokana na kuguswa kwa nyaya hizo.
KIBAHA
Wananchi Mjini Kibaha
wamemuua mtu mmoja aliyefahamika kwa majina ya Michael Wiliam maarufu kama Michael Dada wakimtuhumu kuwateka
watoto wa kike wawili ambao ni wanafunzi kwa lengo la kuwabaka.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari mjini
Kibaha, mkoani Pwani na Kamanda wa Polisi mkoani Pwani Bonaventura Mushongi wananchi
hao wenye hasira walimshambulia mtu huyo sehemu mbalimbali za mwili na
kumsababishia kifo.
Amesema mtoto wa kwanza aliyehusika katika utekaji nyara huo ana
umri wa miaka 11 akiwa anasoma katika Shule ya Msingi Kibaha na wa pili ana
umri wa miaka sita akiwa ni mwanafunzi wa Shule ya Chekechea ya Mama Kawili,
wote wakiwa wanaishi na wazazi wao eneo la Picha ya Ndege.
Kamanda Mshongi , amesema kuwa watoto hao walikubali na kuanza
kuongozana naye lakini wakiwa njiani ghafla lilitokea gari aina ya Toyota Noah
lenye rangi nyeusi ambalo namba zake hazikuweza kufahamika mara moja, na
kusimama walipo watoto hao na baadaye walishuka watu waliofunika sura zao kuwabeba watoto hao na kuwaingiza
katika gari huku gari hilo likiondolewa kwa kasi kuelekea upande lilipo pori la
Shirika la Elimu Kibaha karibu na Shule ya Sekondari ya Tumbi.
Hata hivyo Kamanda Mshongi
amebainisha kuwa uchunguzi uliofanywa na Jeshi la Polisi umebaini kuwa
Wiliam alikuwa mhalifu mzoefu na alikuwa akifanya matukio mara kwa mara ikiwemo
ubakaji na wizi wa mifugo.
MAGEREZA
Mkuu
wa magereza Jenerali John Minja amezuia
kupandishwa vyeo kwa askari kadhaa wa jeshi la magereza ambao wamehitimu mafunzo katika chuo cha Fubila kilichopo wilayani Rungwe mkoani Mbeya baada ya kubaini kuwa na kasoro ikiwa ni pamoja na utoro na
kushindwa kufuatilia kikamilifu mafunzo ya uongozi wa daraja la kwanza.
Jenerali
Minja ametoa kauli hiyo wakati akifunga mafunzo ya uongozi wa daraja la
kwanza kozi namba 22
kwa wahitimu waliofika 80 katika chuo cha Fubila.
Mkuu
wa jeshi la magereza nchini jenerali
Jihn Minja ametangaza rasmi utaratibu mpya wa upandishwaji wa vyeo kwa askari
wa jeshi hilo na hii ni baada ya kubainika kuwa baadhi ya askari wamekuwa
wakitoroka mafunzo.
Kwa
upande wake katibu mkuu wa wizara ya mambo ya ndani ya nchi meja Jenerali Polojest
Lwegasila ametoa maelekezo ya kuheshimu misingi ya kazi.
Na
Veronica /Mhariri Twimanye Chanzo TBC
Umoja wa
Mataifa umehimiza taifa hilo kuheshimu haki za kimsingi za kibinadamu nchini
humo.
Umoja wa
Mataifa pia unasema kuwa watu wengine 85 wametiwa mbaroni katika mji mkuu wa Lubumbashi, baada ya makabiliano makali
kati ya maafisa wa usalama na wafuasi wa vyama vya upinzani siku ya Ijumaa.
Uchaguzi
unatarajiwa mnamo Novemba, lakini tume ya uchaguzi inasema kuwa uchaguzi huo
utacheleweshwa.
Upande wa
upinzani unamlaumu rais Joseph Kabila, ambaye haruhusiwi kikatiba kugombea kiti
hicho tena, kwa kuchelewesha uchaguzi huo makusudi.
Wakati huohuo
Marekani imekosoa Urusi kwa kuitisha
mkutano maalumu wa Baraza Kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa ikisema hatua hiyo
ya Urusi kutaka kuwakosoa Marekani bila sababu maalumu.
Urusi inasema
kuwa wanajeshi 60 wa Syria waliuawa
katika shambulio hilo la Kaskazini Mashariki mwa Syria.
Makao Makuu
ya Kijeshi yanasema kuwa ndege hizo zilidhania kuwa zilikuwa zikishambulia
kambi za makundi ya Islamic State, ambazo Marekani inasema zilikuwa zikitafuta
kwa siku kadhaa.
Lakini Urusi
inasema kuwa Marekani walikuwa na lengo la kuwasaidia wanachama wa Islamic
State na kuongezea kuwa mapatano yake na Marekani kuhusiana na usitishaji wa
mapigano umehatarishwa.
Hakuna habari
za kuthibitisha idadi ya watu waliouawa.
Post a Comment